-
Serikali ya Somalia imechukua hatua gani katika kukabiliana na kujitenga kwa Somaliland?
Jan 21, 2026 04:28Kufuatia kuongezeka harakati za watu wanaotaka kujitenga huko Somaliland baada ya kutambuliwa rasmi na utawala wa Kizayuni wa Israel, serikali ya Somalia imechukua hatua mpya za kukabiliana na harakati hizo katika eneo hilo.
-
Rais wa Somalia atoa wito kwa Somaliland kushiriki katika mazungumzo
Jan 18, 2026 09:05Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amewatolea wito maafisa wa Somaliland kushiriki katika mazungumzo na serikali yake; akisema kuwa yuko tayari kuafikiana katika masuala yote isipokuwa "umoja wa nchi."
-
Magaidi 30 wa al-Shabaab wauawa na vikosi vya Somalia, Uganda na AU
Jan 15, 2026 22:43Vikosi vya Somalia, Uganda na Umoja wa Afrika (AU) jana Alhamisi viliwaangamiza zaidi ya wanamgambo 30 wa al-Shabaab, na kujeruhi wengine kadhaa wakati wa operesheni ya pamoja huko kusini mwa Somalia.
-
Jeshi la Somalia laangamiza magaidi 17 wa al-Shabaab
Jan 14, 2026 02:56Wizara ya Ulinzi wa Somalia imesema kwamba, Jeshi la Kitaifa la nchi hiyo limewaua magaidi 17 wa al-Shabaab katika operesheni ya anga iliiyofanyika kusini mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Somalia: Israel kuwahamishia kwa nguvu Wapalestina Somaliland ni kinyume cha sheria za kimataifa
Jan 11, 2026 03:26Waziri wa Ulinzi wa Somalia, Ahmed Moalim Fiqi, ameishutumu Israel kwa kupanga kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina wa Ukanda wa Gaza na kuwapeleka katika eneo lililojitenga la Somaliland, akiukashifu mpango huo alioutaja kuwa ni "ukiukaji mkubwa" wa sheria za kimataifa.
-
Somalia yakanusha madai ya Marekani ya kutwaa chakula cha WFP
Jan 08, 2026 22:53Somalia jana Alhamisi ilikanusha madai ya Marekani kwamba maafisa wa eneo hilo wametwaa bidhaa za chakula kutoka katika ghala la shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), huku Washington ikisimamisha misaada kwa Mogadishu kusubiri uchunguzi.
-
Somalia yapokezwa uenyekiti wa kiduru wa Baraza la Usalama la UN
Jan 03, 2026 02:33Somalia jana Ijumaa ilichukua urais wa zamu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kipindi cha mwezi huu wa Januari, ikiwa ni mara ya kwanza kwa nchi hiyo kushikilia wadhifa huo tangu ilipohudumu mara ya mwisho katika baraza hilo mwaka 1971-72.
-
Jeshi la Somalia laangamiza makumi ya magaidi wa al-Shabaab
Jan 01, 2026 23:17Makumi ya wanamgambo wa kundi la kigaidi la al-Shabaab lenye misimamo ya kufurutu ada , wameangamizwa katika operesheni ya wanajeshi wa Somalia.
-
Somaliland yajitoa kimasomaso, yakanusha kuafiki kujengwa kambi za kijeshi za Israel
Jan 01, 2026 23:16Eneo la Somaliland la kaskazini mwa Somalia limekanusha madai kwamba lilikubali kuwa mwenyeji wa vituo vya kijeshi vya Israel na kuwapokea Wapalestina waliofurushwa kutoka Gaza ili kutambuliwa na Israel.
-
Rais wa Somalia: Somaliland inashirikiana na Israel dhidi ya Wapalestina
Dec 31, 2025 22:56Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amezinukuu ripoti za kiitelijinsia na kusema kuwa eneo lililojitenga la na nchi hiyo la Somaliland limekubali kuwapokea Wapalestina na kuanzishwa kambi ya kijeshi ya Israel katika eneo hilo mkabala wa kutambuliwa rasmi na Israel.