-
UN yamuwekea vikwazo Waziri wa Ulinzi wa Sudan Kusini
May 27, 2018 09:17Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetangaza kumuwekea vikwazo Waziri wa Ulinzi wa Sudan Kusini, Kuol Manyang Juk kutokana na kile lilichodai kuwa ni kitendo cha afisa huyo wa Juba kukiuka makubaliano ya usitishaji vita.
-
Umoja wa Afrika waitisha mkutano kujadili mgogoro wa mpakani wa Sudan na Sudan Kusini
May 23, 2018 23:39Umoja wa Afrika utafanya mkutano kati ya Sudan na Sudan Kusini kwa lengo la kutatua mgogoro kuhusu eneo la mpakani la Abyei.
-
Zaidi ya watoto 200 waachiliwa huru na makundi ya wabeba silaha Sudan Kusini
May 19, 2018 09:12Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, zaidi ya watoto 200 waliokuwa mikononi mwa makundi ya wabeba silaha huko Sudan Kusini wameachiliwa huru.
-
UN yatuma askari zaidi katika jimbo la Unity, Sudan Kusini
May 17, 2018 09:38Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) kimetuma makumi ya askari wa ziada katika jimbo la Unity ili kuwadhaminia usalama raia wanaolengwa katika vita kati ya askari wa jeshi la serikali na magenge ya waasi.
-
UN: Wakimbizi 15,000 kutoka Sudan Kusini, DRC wameingia Uganda Aprili
May 12, 2018 23:46Ripoti mpya ya Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR imebainisha kuwa, wakimbizi 15,000 hususan kutoka nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Sudan Kusini wameingia nchini Uganda mwezi uliopita pekee wa Aprili.
-
UN yaonya kuhusu hatari ya kuongezeka machafuko Sudan Kusini
Apr 28, 2018 23:07Mkuu wa timu ya Umoja wa Mataifa ya kusimamia amani Sudan Kusini ametahadharisha kuhusu kuongezeka machafuko katika kipindi hiki cha kukaribia mazungumzo ya amani nchini humo.
-
Wafanyakazi 10 wa UN watoweka Sudan Kusini
Apr 26, 2018 23:30Afisa mmoja wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa wafanyakazi wasiopungua 10 wa umoja huo nchini Sudan Kusini wametoweka na hawajulikani waliko.
-
Rais wa Sudan Kusini apinga wito wa wapinzani wa kujiuzulu
Apr 25, 2018 09:27Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amepinga wito uliotolewa na wapinzani nchini humo waliomtaka ajiuzulu kama sehemu ya jitihada za kuhitimisha vita vya ndani. Rais Kiir ameyatuhumu makundi yanayopinga serikali yake kwa kuwasilisha matakwa yasiyo ya kimantiki katika mazungumzo ya amani.
-
Askari wa UN watuhumiwa kuwabaka watoto Sudan Kusini
Apr 24, 2018 12:15Wanajeshi wa Umoja wa Mataifa kutoka Nepal wanatuhumiwa kuwabaka watoto wadogo nchini Sudan Kusini.
-
UNICEF: Watoto wengi waliokuwa jeshini Sudan Kusini wameachiliwa huru
Apr 20, 2018 02:51Watoto zaidi ya 200 waliokuwa wamesajiliwa kama wanajeshi katika makundi ya wapiganaji nchini Sudan Kusini wameachiliwa huru.