-
Walionaswa na meli ya madawa ya kulevya yenye usajili wa Tanzania watiwa hatiani
Jul 14, 2016 23:41Watu wawili raia wa Uturuki walionaswa mwaka jana kwenye ufukwe wa Aberdeen, Scotland na meli iliyokuwa imebeba tani tatu za dawa za kulevya aina ya cocaine huku ikiwa na usajili wa nchini Tanzania, wamekutwa na hatia mahakamani nchini Scotland.
-
Waislamu Tanzania watakiwa kusherehekea Idul Fitr kwa namna inayokubalika
Jul 05, 2016 02:48Huku Waislamu wakijiandaa kwa ajili ya sherehe za Iddil-Fitri kutokana na kuelekea kumalizika mwezi mtukufu wa Ramadhani, Waislamu nchini Tanzania wametakiwa kuadhimisha sherehe hizo kwa Amani na utulivu. Hayo yamesemwa na Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa Salum, ambapo pia amewataka Waislamu hao kujiepusha kumuasi Mwenyezi Mungu katika sherehe hizo….
-
Sheikh Hemedi Jalala: Walimwengu wanapaswa kupinga ukandamizaji dhidi ya Wapalestina
Jul 02, 2016 00:08Walimwengu wametakiwa kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina na kupaza sauti za kupinga dhulma, unyanyasaji na mauaji yanayofanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya wananchi wa Palestina.
-
Watanzania waadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds
Jul 01, 2016 10:57Wananchi wa Tanzania wameadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds hii leo ambayo ni Ijumaa ya mwisho ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani ikiwa ni katika kuonyesha mshikamano wao na muqawama wa wananchi wa Palestina mbele ya maghasibu Wazayuni.
-
Rais Magufuli: Polisi ongezeni juhudi kiutendaji kumaliza ujambazi
Jun 26, 2016 03:30Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania amewataka polisi wa nchi hiyo kuongeza juhudi katika utendaji kazi wao ili kukabiliana na uhalifu nchini.
-
Mabaki ya Ndege yaliyopatikana Pemba, Tanzania kuchunguzwa iwapo ni ya ndege ya Malaysia
Jun 24, 2016 03:36Uchunguzi umeanzishwa kubaini iwapo kipande cha mabaki ya ndege kilichopatikana kisiwani Pemba nchini Tanzania ni kile cha ndege ya Malaysia aina ya Boeing 777 , Nambari MH370 iliyotoweka Machi 2014 au la.
-
Mwinyi: Tofauti za kidini zisiwagawanye Watanzania
Jun 17, 2016 23:23Rais mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi ameshutumu vikali kile alichokitaja kuwa udini na kuwataka Watanzania kutoruhusu tofauti zao za kidini na kimadhehebu kuwa chanzo cha mgawanyiko miongoni mwao.
-
Mamia ya wasichana wa Kitanzania walioko India, Thailand, Oman Saudia nk kurejeshwa nchini
Jun 11, 2016 00:00Serikali ya Tanzania imesema kuwa, itawarudisha nchini mamia ya wasichana raia wa nchi hiyo waliokwama nchini India na mataifa mengine baada ya taasisi zilizowachukua kwenda kuwatafutia ajira, kukiuka mikataba yao na kuwalazimisha kufanya kazi tofauti ikiwemo ya ukahaba.
-
NEC Tanzania: Hatukuwataka waangalizi wa uchaguzi kuangalia wa ZNZ ila wa bara
Jun 05, 2016 00:07Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Tanzania (NEC) imetoa radiamali yake juu ya ripoti ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana 2015, iliyowasilishwa hivi karibuni na ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi wa Umoja wa Ulaya (EU).
-
Tanzania: Wakaazi wa kijiji kulikojiri mauaji Tanga wahama
Jun 03, 2016 10:14Wakaazi wa kijiji cha Kibatini mkoani Tanga huko Tanzania wamekihama kijiji chao kufuatia mauaji ya kutisha yaliyotokea katika eneo hilo.