Mar 24, 2016 16:23
Rais mteule wa Zanzibar, Dakta Ali Mohamed Shein ameapishwa leo kushika hatamu ya uongozi visiwani humo. Dakta Shein ameapishwa leo kufuatia ushindi alioupata Jumapili iliyopita wa kura 299,982 sawa na asilimia 91.4 ya kura zote halali 328,327 zilizopigwa katika uchaguzi marudio.