-
Guterres ataka uchunguzi huru wa kushambuliwa meli za mafuta Bahari ya Oman
Jun 15, 2019 03:45Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa mwito wa kufanyika uchunguzi huru wa tukio la kushabuliwa meli za mafuta katika Bahari ya Oman.
-
UN: 60% ya wananchi wa Sudan Kusini wanakabiliwa na baa la njaa
Jun 15, 2019 03:28Mashirika ya Umoja wa Mataifa yamesema jumla ya watu milioni 7 sawa na asilimia 60 ya jamii nzima ya Sudan Kusini wanakabiliwa na baa la njaa.
-
UN: Idadi ya waliouawa Darfur nchini Sudan ni watu 17
Jun 13, 2019 21:58Umoja wa Mataifa umethibitisha kuwa kwa akali watu 17 wameuawa katika kijiji cha Deleij katikati mwa jimbo la Darfur, magharibi mwa Sudan.
-
Tunisia na Niger zachaguliwa kuwa wanachama wa Baraza la Usalama
Jun 08, 2019 02:26Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Ijumaa lilizichagua nchi tano wanachama wa umoja huo kuwa wanachama wasio wa kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuanzia mwezi Januari mwakani.
-
UN yapuuzilia mbali mkutano wa Manama wa kujadili mpango wa "Muamala wa Karne"
May 31, 2019 03:43Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa hautashiriki katika mkutano wa Kiuchumi uliopangwa kufanyika Manama mji mkuu wa Bahrain khususan kujadili mpango kwa jina la "Muamala wa Karne."
-
Onyo la Umoja wa Mataifa kuhusu hatari ya kutumika silaha za nyuklia
May 24, 2019 02:35Kuwepo maghala ya silaha hatari za nyuklia katika pembe tofauti za dunia, kuongezwa na kuimarishwa silaha hizo na vilevile kujiunga nchi mpya na kundi la nchi zinazomiliki silaha hizo ni jambo linalohatarisha amani na uslama wa dunia.
-
UN yamteua afisa kupambana na Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
May 23, 2019 06:47Umoja wa Mataifa umemteuwa Mratibu wa Hatua za Dharura za Kukabiliana na Maradhi ya Ebola ambaye atasaidia kuimarisha jitihada za kukomesha kuenea maradhi ya Ebola yaliyodumu kwa miezi kumi sasa huko Kongo DRC na kuua watu zaidi ya 1,200.
-
Indhari ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali inavyozidi kuwa mbaya nchini Libya
May 23, 2019 03:43Kuendelea vita nchini Libya kumezidisha machafuko na mgogoro katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kiasi kwamba Ghassan Salamé, mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya amesema katika ripoti yake ya hivi karibuni kabisa kwamba, hatoi tahadhari kuhusu kutokea vita vya ndani na vya umwagaji damu tu, bali anatoa onyo la kusambaratika vipande vipande Libya.
-
Libya katika ncha ya kutumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe
May 22, 2019 03:26Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya ameonya kuwa, taifa hilo lenye utajiri wa mafuta liko katika ncha ya kutumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vitaigawa nchi hiyo mapande mapande.
-
UN: Kuna uwezekano mkubwa wakati huu wa kutumika silaha za nyuklia
May 22, 2019 02:00Mkurugenzi wa Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Utafiti wa Upokonyaji Silaha UNIDIR amesema hatari na uwezekano wa kutumika silaha za nyuklia duniani hii leo uko juu kuliko wakati mwingine wowote ule.