-
Uturuki yaanza kutuma vikosi vya jeshi lake nchini Libya
Jan 06, 2020 04:30Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema vikosi vya jeshi la nchi hiyo vimeanza kuelekea nchini Libya, kushirikiana na Serikali ya Muafaka wa Kitaifa Libya (GNA) inayoongozwa na Waziri Mkuu Fayez al-Sarraj.
-
Bunge la Uturuki laidhinisha kutumwa askari wa nchi hiyo Libya
Jan 02, 2020 23:23Bunge la Uturuki limepasisha muswada wa sheria inayoruhusu kutumwa wanajeshi wa nchi hiyo huko Libya.
-
Uturuki: Hatutapeleka askari Libya ikiwa vikosi vya Haftar vitasitisha mashambulio dhidi ya Tripoli
Jan 02, 2020 00:23Makamu wa Rais wa Uturuki Fuat Oktay amesema, nchi yake haitapeleka askari Libya ikiwa vikosi vya kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na Khalifa Haftar vitasitisha mashambulio dhidi ya mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli.
-
Arab League yaonya juu ya kutumwa majeshi ajinabi Libya
Jan 01, 2020 04:30Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imeziasa pande hasimu za kisiasa nchini Libya kujiepusha na hatua yoyote ambayo itachochea kutumwa vikosi vya nchi za kigeni katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Khalifa Haftar anajaribu kueneza wigo wa kimataifa wa mgogoro wa Libya
Jan 01, 2020 04:22Baada ya kupinduliwa utawala wa Muammar Gaddafi huko Libya mwaka 2011, nchi hiyo ilitumbukia katika vita vya ndani na hivi sasa kuna serikali mbili hasimu, moja ya mashariki na nyingine ya magharibi mwa nchi hiyo ambapo vikosi vya pande hizo mbili vinaendelea kupigana,
-
Uturuki yatangaza kuwa tayari kutuma wanajeshi wake Libya kuisaidia serikali ya Sarraj
Dec 23, 2019 03:44Makamu wa Rais wa Uturuki Fuat Oktay ametangaza kuwa, 'iwapo serikali ya muafaka wa kitaifa Libya itawasilisha ombi rasmi, Uturuki iko tayari kutuma wanajeshi wake katika nchi hiyo ya Afrika Kaskazini.
-
Kikosi cha Haftar chateka nyara meli ya Uturuki pwani mwa Libya
Dec 22, 2019 08:07Kikosi cha linalojiita jeshi la taifa la Libya chini ya uongozi wa Jenerali Khalifa Haftar kimeteka nyara meli ya Uturuki katika maji ya Bahari ya Mediterania na kuipeleka katika bandari ya Ra's Al Hilal huko mashariki mwa Libya.
-
Rais Putin wa Russia ataka kuhitimishwa mgogoro wa Libya
Dec 19, 2019 09:25Rais Vladimir Putin wa Russia amesema angependa kuona mgogoro wa Libya unapatiwa ufumbuzi na mazungumzo baina ya pande mbili hasimu katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika yanaanza.
-
Uturuki kujibu mapigo kwa kutambua kuuliwa wakazi wa asili wa Marekani kuwa ni 'mauaji ya kimbari'
Dec 17, 2019 09:11Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema, nchi yake itachukua hatua ya kuyatambua mauaji ya mamilioni ya wakazi wa asili wa Marekani kuwa ni "mauaji ya kimbari" ili kujibu mapigo kwa hatua ya karibuni iliyochukuliwa na serikali ya Washington ya kuyaelezea mauaji ya halaiki ya Waarmenia yaliyofanywa na utawala wa zamani wa Uturuki wa Dola la Othmaniya kuwa ni mauaji ya kimbari.
-
Serikali ya muda ya Libya yaeleza wasiwasi wake kuhusu mapatano ya Sarraj na Erdogan
Dec 08, 2019 23:10Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali ya muda yenye makao yake mashariki mwa Libya amesema kuwa wanatiwa wasiwasi na mapatano yaliyofikiwa kati ya serikali ya umoja wa kitaifa ya nchi hiyo yenye makao makuu yake mjini Tripoli, na Uturuki.