-
Kadhaa wauawa katika shambulio la al-Shabaab, Garissa Kenya
Jul 14, 2025 11:42Watu wawili wameuawa huku wengine kadhaa wakijeruhiwa katika shambulio linaloshukiwa kuwa la magaidi wa al-Shabaab katika Kaunti ya Garissa, kaskazini mashariki mwa Kenya.
-
Mkuu wa Jeshi la Uganda: US imeanzisha mazungumzo ya siri na al-Shabaab Somalia
Jul 14, 2025 11:03Mkuu wa Jeshi la Uganda ametoa wito wa kuondolewa kikamilifu wanajeshi wa Umoja wa Afrika kutoka Somalia, akidai kuwa Marekani imeanzisha mazungumzo ya siri na kundi la kigaidi la al-Shabaab.
-
Rasmi; Rais wa Cameroon, Paul Biya (92) kugombea muhula mwingine katika uchaguzi ujao
Jul 14, 2025 09:26Rais wa sasa wa Cameroon, Paul Biya ametangaza kuwa atagombea muhula wa nane katika uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika Oktoba 12, na hivyo kuhitimisha uvumi wa miezi kadhaa wa iwapo atawania au la.
-
Baadhi ya Waislamu Kenya wapendekeza Kadhi Mkuu ajaye atoke nje ya Pwani
Jul 14, 2025 03:26Baada ya kupita siku chache tu tangu alipoaga dunia Kadhi Mkuu wa Kenye Sheikh Abdulhalim Hussein Athman, baadhi ya Waislamu wamependekeza kadhi ajaye atoke nje ya eneo la Pwani.
-
Mkuu wa Mawaziri Kenya atofautiana na Rais Ruto kuhusu kuwapiga risasi waandamanaji
Jul 13, 2025 23:43Mkuu wa Mawaziri wa Mawaziri nchini Kenya, Musalia Mudavadi ametofautiana na Rais William Ruto kuhusu wito wake wa kupigwa risasi viijana wanaoandamana kupinga sera za serikali yake na amevitaka vyombo vya usalama visiwaumize Wakenya wakati wa maandamano.
-
Muhammadu Buhari, rais wa zamani wa Nigeria afariki dunia Uingereza alikokuwa matibabuni
Jul 13, 2025 14:57Muhammadu Buhari, rais wa zamani wa Nigeria aliyewahi pia kuitawala nchi hiyo kijeshi amefariki dunia mjini London, Uingereza alikokuwa kipatiwa matibabu akiwa na umri wa miaka 82.
-
Nigeria yawafunga watu 44 waliofadhili kundi la kigaidi la Boko Haram
Jul 13, 2025 10:28Serikali ya Nigeria imewahukumu watu 44 kifungo cha hadi miaka 30 jela kwa makosa ya kufadhili ugaidi, msemaji wa shirika la kupambana na ugaidi nchini humo amebaini.
-
Watoto watatu wa Kisuadani ni miongoni mwa raia 11 waliouawa na waasi wa RSF huko Kordofan
Jul 13, 2025 09:52Raia wasiopungua 11, wakiwemo watoto watatu, wameuawa katika shambulizi la kikosi cha wanamgambo wa Jeshi la Msaada wa Haraka (RSF) katika jimbo la Kordofan Kaskazini, magharibi mwa Sudan, kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa madaktari wa eneo hilo leo Jumapili.
-
DRC yataka maelezo kutoka Uganda kuhusu kufunguliwa mpaka wa Bunagana
Jul 12, 2025 23:41Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetaka maelezo kutoka kwa serikali ya Uganda, kuhusiana na kufunguliwa kwa mpaka wa Bunagana, katika eneo linalodhibitiwa na waasi wa M23.
-
Ethiopia kuitosa sarafu ya dola ya US katika miamala ya biashara?
Jul 12, 2025 13:03Wizara ya Fedha ya Ethiopia imesema kuwa nchi hiyo ya Afrika Mashariki inafanyia kazi hatua za kuiruhusu kufanya biashara kwa kutumia sarafu tofauti isiyo dola ya Marekani, na kwamba kuna nchi ambazo imefikia makubaliano nazo katika suala hili kwa nyakati tofauti.