-
Kambi ya upinzani Kenya yapinga uteuzi wa Rais Ruto wa makamishna wa IEBC
May 10, 2025 08:49Ripoti kutoka Kenya zinasema, watu watano kati ya saba walioteuliwa na Rais William Ruto kusimamia Uchaguzi Mkuu ujao wana uhusiano wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja na kiongozi huyo pamoja na mshirika wake katika Serikali Jumuishi, Raila Odinga, hali ambayo imezua malalamiko kutoka kambi ya upinzani kwamba walioteuliwa hawatakuwa maamuzi huru.
-
MSF: Vita nchini Sudan vimeharibu sekta ya afya
May 10, 2025 08:48Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limeonya kwamba hali ya afya katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum, inazidi kuwa mbaya kutokana na vita, na kukosekana huduma za afya za kimsingi na za kuokoa maisha ya watu.
-
Rais wa Burundi azindua kampeni ya uchaguzi wa 2025 wa wabunge na wilaya
May 10, 2025 03:24Rais Evariste Ndayishimiye wa Burundi jana Ijumaa alizindua rasmi kampeni ya uchaguzi wa pamoja wa wabunge na wilaya, unaotarajiwa kufanyika Juni 5, akiwa Gitega, mji mkuu wa kisiasa wa nchi hiyo.
-
Benki Kuu za EAC zakadiria ukuaji wa uchumi wa asilimia 5.8 mwaka 2025
May 10, 2025 02:11Benki Kuu za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jana Ijumaa zilikadiria kuwa, uchumi wa ukanda huo kwa mwaka huu wa 2025 utakuwa kwa asilimia 5.8.
-
Baraza la Usalama laongeza muda wa kuhudumu UNMISS Sudan Kusini
May 09, 2025 07:05Baada ya majuma kadhaa ya mazungumzo makali, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeongeza muda wa kikosi cha kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS, kwa mwaka mmoja mwingine, huku likitaka kusitishwa mara moja kwa mapigano kati ya pande hasimu.
-
Umoja wa Mataifa wapunguza msaada wa kibinadamu DRC
May 09, 2025 07:01Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, umepunguza kwa karibu nusu malengo yake ya misaada ya kibinadamu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
DRC: Chama cha Kabila chasema kimerejea kazini licha ya kupigwa marufuku
May 08, 2025 22:51Chama cha Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila kimesema kuwa, kitaendelea na shughuli zake kama kawaida licha ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo kupiga marufuku shughuli zake hizo.
-
Rais wa Algeria asema nchi yake haitasahau uhalifu wa ukoloni wa Ufaransa
May 08, 2025 07:26Rais Abdelmadjid Tebboune wa Algeria, amesisitiza kwamba suala la kumbukumbu ya kitaifa kuhusiana na utawala wa kikoloni wa Ufaransa nchini humo “halitakuwa jambo la kusahauliwa au kukanwa.”
-
Jiji la Port Sudan lashambuliwa kwa ndege isiyo na rubani kwa siku ya tano mfululizo
May 08, 2025 07:14Jiji la Port Sudan, mashariki mwa Sudan, Alhamisi asubuhi limekumbwa na shambulio jipya la ndege isiyo na rubani (drone) kwa siku ya tano mfululizo, huku mapigano makali yakiendelea kati ya jeshi na waasi wa RSF.
-
Afrika Kusini Kuendesha Mkutano wa Kilele wa G20 kwa mafanikio hata bila uwepo wa Marekani
May 08, 2025 07:09Afrika Kusini itahakikisha Mkutano wa Kilele wa G20 unafanikiwa, iwe Marekani itahudhuria au la, amesema Makamu wa Rais wa nchi hiyo, Paul Mashatile.