-
Rwanda yapiga marufuku mashirika, asasi kushirikiana na Ubelgiji
Mar 28, 2025 03:54Serikali ya Rwanda imeyapiga marufuku mashirika yote ya kimataifa na ya kitaifa yasiyo ya kiserikali (NGOs) na mashirika yanayofanya kazi nchini humo kushirikiana na serikali ya Ubelgiji na mashirika yake tanzu.
-
Watalii kadhaa wafa maji baada ya nyambizi kuzama katika Bahari Nyekundu
Mar 28, 2025 03:42Raia sita wa Russia wamepoteza maisha huku watalii 39 wa kigeni wakiokolewa wakati nyambizi ya kitalii ilipozama kwenye eneo la kitalii la Hurghada kwenye maji ya Bahari Nyekundu pwani ya Misri.
-
Mkuu wa UN atiwa wasiwasi na hali kuzidi kuwa tete Sudan Kusini
Mar 28, 2025 03:30Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema anasikitishwa sana na kuendelea kushtadi taharuki na hali ya mambo nchini Sudan Kusini.
-
Ndege ya Al-Burhan yatua Khartoum kwa mara ya kwanza baada ya kuanza vita, atangaza kufukuzwa RSF
Mar 27, 2025 07:47Kamanda wa jeshi la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, alirejea Khartoum jana, Jumatano, Kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa wa mji huo, ikiwa ni kwa mara ya kwanza tangu uwanja huo ugeuke kuwa uwanja wa vita Aprili 2023.
-
Magaidi washambulia kambi za jeshi Nigeria, Cameroon na kuua askari 16
Mar 27, 2025 07:38Watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa magenge ya kigaidi wamefanya mashambulizi yaliyoratibiwa dhidi ya kambi ya jeshi la Cameroon karibu na Ziwa Chad na dhidi ya kituo cha kijeshi kaskazini mashariki mwa Nigeria, na kuua takriban wanajeshi 16.
-
Jenerali Tchiani kuiongoza Niger kwa mpito wa miaka 5
Mar 27, 2025 07:37Kiongozi wa kijeshi wa Niger ameapishwa rasmi kuwa rais wa nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika kwa kipindi cha mpito cha miaka mitano.
-
Hali yazidi kuwa tete Sudan Kusini baada ya Makamu wa Rais Machar kukamatwa, UN yaonya
Mar 27, 2025 02:26Chama kikuu cha upinzani nchini Sudan Kusini kimesema, kiongozi wake Riek Machar, ambaye ni Makamu wa Rais wa nchi hiyo amekamatwa, huku Umoja wa Mataifa ukizitaka pande zote kuheshimu makubaliano ya mwaka 2018 yaliyomaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
-
Umoja wa Afrika wataka kufadhiliwa zaidi juhudi za amani nchini Somalia
Mar 26, 2025 22:50Mwenyekiti mpya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika AU, Mahmoud Ali Youssouf, ametoa mwito kwa jamii ya kimataifa kuongeza misaada yao ya kufanikisha juhudi za kuleta utulivu nchini Somalia.
-
UN yasikitishwa na kuendelea mashambulizi dhidi ya raia nchini Sudan
Mar 26, 2025 22:50Msemaji Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, kuendelea mashambulizi dhidi ya raia nchini Sudan, ikiwa ni pamoja na shambulio baya la anga lililofanywa kwenye soko la Darfur Kaskazini, kumeutia wasiwasi mkubwa umoja huo.
-
Rais Ruto: Mwanasheria Mkuu aliyefutwa kazi alichelewesha tume ya wakfu wa Waislamu
Mar 26, 2025 09:21Rais William Ruto wa Kenya amemkosoa hadharini aliyekuwa Mwanasheria Mkuu Justin Muturi, akitaja kipindi chake cha uongozi kuwa "kisichofaa" katika kushughulikia masuala muhimu ya kisheria, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa Tume ya Wakfu wa Kiislamu. Kwa muda mrefu uanzishwaji wa mfuko huo umekuwa kilio cha Waislamu wa Kenya.