-
Burkina Faso yatangaza viza bila malipo kwa Waafrika wote
Sep 12, 2025 22:58Burkina Faso imetangaza kuwa viza ya kuingia nchini humo kwa raia wote wa nchi za Afrika sasa itakuwa bila malipo, ikiwa ni sehemu ya hatua kadhaa zilizopitishwa na Baraza la Mawaziri katika kikao chake cha kila wiki kilichoongozwa na Rais wa Mpito, Kapteni Ibrahim Traoré.
-
Nchi za Afrika zalaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Doha
Sep 12, 2025 22:57Nchi kadhaa za Afrika pamoja na Umoja wa Afrika (AU) zimetoa taarifa kali kulaani mashambulizi ya anga yaliyofanywa na utawala wa Israel siku ya Jumanne, yaliyolenga uongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Kupigania Ukombozi wa Palestina, Hamas, nchini Qatar, wakionya kuwa kitendo hicho ni uvunjaji wa wazi wa mamlaka ya taifa hilo la Ghuba ya Uajemi.
-
Indhari ya UN: Mafuriko makubwa Sudan Kusini yaweza kuathiri zaidi ya watu milioni moja
Sep 12, 2025 22:57Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi (UNHCR) limetoa tahadhari kali kuhusu mafuriko makubwa yanayoendelea nchini Sudan Kusini, likisema kuwa tayari yameathiri watu wapatao 273,000 mwaka huu, na huenda yakawaathiri zaidi ya milioni moja katika miezi ijayo.
-
Africa CDC: Kwa muda wa wiki moja, kesi za Ebola zimeongezeka zaidi ya maradufu mkoani Kasai, DRC
Sep 12, 2025 06:57Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Maradhi, (Africa CDC) kimetangaza kuwa, idadi ya watu wanaoshukiwa kuwa na ugonjwa hatari wa Ebola katika jimbo la Kasai kusini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imeongezeka zaidi ya maradufuu katika muda wa wiki moja tangu ulipothibitishwa mripuko mpya wa ugonjwa huo katika eneo hilo.
-
Sudan Kusini yamshtaki Makamu wa Rais Machar kwa uhaini, mauaji
Sep 12, 2025 03:16Riek Machar, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini amefunguliwa mashitaka ya mauaji, uhaini na uhalifu dhidi ya binadamu.
-
Mwendesha mashtaka ataka Felicien Kabuga arejeshwe Rwanda
Sep 11, 2025 23:48Mwendesha mashitaka wa kitengo cha Mahakama ya kimataifa ya mauaji ya kimbari ya Rwanda (ICTR) ametoa ombi la kurejeshwa Rwanda Felicien Kabuga anayekabiliwa na mashtaka ya mauaji ya Rwanda.
-
Araghchi katika mazungumzo na Mufti Mkuu wa Tunisia: Kukomeshwa mauaji ya halaiki huko Gaza kunahitajia ushirikiano wa Umma wa Kiislamu
Sep 11, 2025 09:20Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika kikao na Mufti Mkuu wa Tunisia kwamba: "Kukomeshwa mauaji ya halaiki ya utawala wa Kizayuni huko Gaza na kuzuia kupanuka kwa wigo wa uchokozi wa utawala huo kunahitajia ushirikiano mkubwa wa Umma wa Kiislamu."
-
Utekaji nyara wa wafanyakazi wa misaada huko Sudan Kusini ni zaidi ya maradufu
Sep 11, 2025 07:59Idadi ya wafanyakazi wa misaada waliotekwa nyara nchini Sudan Kusini imeongezeka zaidi ya mara mbili mwaka huu. Takwimu hii imetolewa na maafisa wawili waandamizi wa masuala ya kibinadamu wanaofanya kazi katika makundi ya kimataifa.
-
Afrika Kusini imewahukumu raia 7 wa China miaka 20 jela kila mmoja kwa magendo ya binadamu
Sep 11, 2025 07:33Mahakama moja mjini Johannesburg Afrika Kusini imewahukumu raia saba wa China kifungo cha miaka 20 jela kila mmoja kia mmoja baada ya kuwapata na hatia ya magendo ya binadamu. Raia hao wa China wamekutwa na hatia ya kuwasafirisha watu kutoka Malawi na kuwalazimisha kufanya kazi katika kiwanda kimoja nchini Afrika Kusini.
-
Afrika yataka kuchukuliwa hatua madhubuti ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi
Sep 11, 2025 03:50Afrika inachangia chini ya asilimia 5 ya uzalishaji wa gesi chafuzi duniani lakini inalipa kile ambacho mtaalamu mmoja wa masuala ya hali ya hewa anakiita “gharama kubwa" ya mabadiliko ya hali ya hewa; mada ambayo imetawala katika Mkutano wa Pili wa Hali ya Hewa wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia.