-
Iran yaitaka UN kukomesha mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza
Apr 24, 2024 23:51Mwakilishi wa Iran katika ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Geneva amemwandikia barua mkuu wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu na Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, akiwaomba kuchukua hatua za haraka za kukomesha mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel dhidi ya watu wa Gaza huko Palestina.
-
Kuiwekea vikwazo sekta ya ulinzi ya Iran, zawadi mpya iliyotunukiwa Israel na Magharibi
Apr 24, 2024 23:05Katika hatua uliyochukua ili kuufurahisha utawala wa Kizayuni wa Israel, Umoja wa Ulaya umetangaza kuwa utapanua wigo wa vikwazo ulivyoiwekea sekta ya ulinzi ya Iran.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Taifa la Iran halitasalimu amri mbele ya sera za mabavu
Apr 24, 2024 08:56Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: Taifa kubwa na lenye historia ya miaka mingi la Iran halitasalimu amri mbele ya sera za kidhalimu na za kupenda kujitanua na litafika kwenye upeo mzuri wa mustakabali kwa kugeuza vikwazo kuwa fursa.
-
Kan'ani: Ukiukaji wa haki za binadamu nchini Marekani umeitia wasiwasi dunia
Apr 24, 2024 08:41Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, ukiukaji wa kutisha wa haki ya kupiga kura, uhuru wa kusema na haki za binadamu huko Marekani unawatia wasiwasi mkubwa watu duniani.
-
Sisitizo la Rais wa Iran kwamba Palestina ni suala kuu la Ulimwengu wa Wanadamu
Apr 24, 2024 03:49Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kwa mara nyingine tena kuwa kadhia ya Palestina ndilo suala kuu la Ulimwengu wa Wanadamu.
-
Msemaji wa Serikali ya Iran: Kuna Pengo kubwa kati ya viongozi wa Marekani na maoni ya umma
Apr 24, 2024 02:55Msemaji wa Serikali ya Iran amesema, akizungumzia msaada mpya wa kifedha wa Marekani kwa utawala wa Kizayuni wa Israel, kwamba: Pengo kubwa lililopo kati ya watawala walioathiriwa na Uzayuni na maoni ya umma katika nchi za Magharibi haliwezi kukanushwa tena.
-
Rais Raisi: Israel ikifanya kosa jengine dogo haitabaki tena
Apr 23, 2024 23:15Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika kikao na wasomi wa jimbo wa Punjab nchini Pakistan kwamba iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utafanya kosa jengine dogo na kuivamia ardhi takatifu ya Iran, hali itakuwa tofauti kabisa na hakuna ajuaye kama utawala huo utabaki tena.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran akosoa ufuasi kipofu wa Ulaya kwa Marekani
Apr 23, 2024 08:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekosoa uamuzi wa Umoja wa Ulaya wa kuiwekea Iran vikwazo vilivyo kinyume cha sheria, akisema kuwa watu wa Ulaya hawapaswi kufuata ushauri wa Marekani wa kuuridhisha utawala mtendajinai wa Israel.
-
Raisi: Iran itaendelea kuunga mkono uhuru wa Syria
Apr 23, 2024 05:06Rais wa Iran Ebrahim Raisi amesema Jamhuri ya Kiislamu itasimama kidete pamoja na Syria na itaendelea kuunga mkono uhuru wake na umoja wa ardhi yake.
-
Safari ya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Pakistan
Apr 23, 2024 04:54Ziara ya siku mbili ya Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Pakistan inatathminiwa kuwa ni safari ya kihistoria ambayo inatarajiwa kufungua ukurasa na anga mpya ya uhusiano kati ya Tehran na Islamabad.