-
Wananchi wa Iran leo wanapiga kura kumchagua mrithi wa Rais Ebrahim Raisi
Jun 28, 2024 01:00Wananchi wa Iran waliotimiza masharti ya kupiga kura leo wanaelekea katika vituo vya kupigia kura ili kumchagua Rais mpya atakayemrithi Ebrahim Raisi aliyekufa shahidi katika ajali ya helikopta Mei 19 mwaka huu.
-
Qaani: Raisi, Abdollahian walithibitisha kuwa Iran inaweza kuikabili Marekani
Jun 27, 2024 23:52Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesifu na kupongeza sifa za kipekee walizojipambanua nazo Shahidi Rais Sayyid Ebrahim Rais na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian, kwa kuiunga mkono kambi ya muqawama na kukabiliana na ubeberu wa Marekani.
-
Iran yalaani jaribio la mapinduzi lililofeli Bolivia
Jun 27, 2024 23:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani jaribio la mapinduzi lililofeli nchini Bolivia.
-
Kanani: Iran ni mbeba bendera ya mapambano ya dunia dhidi ya magenge hatari ya mihadarati
Jun 27, 2024 09:12Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza juu ya irada madhubuti ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kupambana na tishio la dunia la madawa ya kulevya.
-
Tehran, mwenyeji wa mkutano wa nafasi ya utambulisho wa asili na muqawama katika kuasisi mfumo mpya duniani
Jun 27, 2024 08:59Mkutano wa kimataifa uliofanyika chini ya anwani ya "Nafasi ya Utambulisho wa Asili na Muqawama Katika Kuasisi Mfumo Mpya Duniani" umefanyika leo hapa Tehran kwa kuhudhuriwa na wataalamu na wanafikra wa kimataifa.
-
Kuongezeka kasi katika ushirikiano wa kimkakati kati ya Iran na Russia
Jun 27, 2024 08:55Uhusiano na ushirikiano wa kistratijia kati ya Iran na Russia umeongezeka na kushika kasi zaidi katika siku za hivi karibuni, na sasa unaingia katika hatua mpya.
-
Zakani ajiondoa katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa rais wa Iran
Jun 27, 2024 08:46Alireza Zakani, mgombea wa kiti cha urais kwa muhula wa 14, leo Alhamisi, tarehe 7 Julai, ametoa tamko akitangaza kujiondoa katika kinyang'anyiro cha kuwania kiti hicho.
-
Barua ya wanazuoni wa Kisunni wa Iran kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kuhusu uchaguzi wa kesho
Jun 27, 2024 04:38Katika barua waliyomuandikia Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, zaidi ya wanazuoni elfu mbili wa Kisunni wa Iran wamesema kuwa uchaguzi wa rais utakaofanyika kesho Ijumaa hapa nchini utaimarisha nguvu na irada ya taifa la Iran.
-
Kuimarika uhusiano wa Iran na Russia kufuatia kusainiwa mkataba wa usambazaji gesi
Jun 27, 2024 02:20Kaimu Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kutiwa saini mapatano ya kusafirisha gesi ya Russia hadi Iran ni hatua muhimu katika mwelekeo wa kuimarisha uhusiano wa nchi mbili na hatua athirifu inayolenga kustawisha uchumi wa eneo.
-
Ghazizadeh Hashemi ajiondoa katika kinyang'anyiro cha urais wa Iran
Jun 26, 2024 23:30Amir-Hossein Ghazizadeh Hashemi, mmoja wa wagombea sita wa kiti cha rais ajaye wa Iran, amejiondoa katika kinyang'anyiro hicho. Uchaguzi huo wa kabla ya wakati wake unafanyika kesho Ijumaa tarehe 28 Juni, 2024.