-
Tehran: Vyombo vya habari vya Magharibi vinajaribu kugeuza kushindwa Israel kuwa ushindi
Apr 20, 2024 04:47Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian amesema kuwa quadcopter tatu za kigeni (videge vigogo visivyo na rubani) zilizotunguliwa na walinzi wa anga wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mji wa kati wa Isfahan hazikusababisha uharibifu wala majeruhi yoyote ndani ya nchi.
-
Iran yalaani veto ya Marekani dhidi ya uanachama kamili wa Palestina UN
Apr 20, 2024 03:13Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kura ya turufu ya Marekani dhidi ya rasimu ya azimio iliyotaka Palestina ipewe uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.
-
Iran na Uturuki zatilia mkazo wajibu wa kukomeshwa haraka mashambulizi huko Ghaza
Apr 19, 2024 23:29Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki wamehimiza na kutilia mkazo udharura wa kukomeshwa mara moja mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Ghaza.
-
Sheikh Akbari: Operesheni ya Ahadi ya Kweli ni Kimbunga cha al Aqsa cha Iran
Apr 19, 2024 07:53Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa Tehran amesema kuwa, operesheni iliyofanywa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kulipiza kisasi jinai za Israel ilikuwa ni kimbunga cha al Aqsa cha Iran dhidi ya utawala wa Kizayuni na ni operesheni ya kujivunia na kujifakharisha nayo.
-
Vyombo vya habari: Iran imetungua ndege tatu zisizo na rubani katika mji wa Esfahan
Apr 19, 2024 04:28Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, mfumo wa ulinzi wa anga wa Iran umetungua ndege tatu ndogo zisizo na rubani katika mkoa wa Esfahan ulioko katikati mwa nchi saa kadha baada ya vyombo vya habari vya Marekani kuwanukuu maafisa waandamizi wa nchi hiyo wakidai kwamba makombora ya utawala wa Kizayuni wa Israel yamepiga eneo la Iran.
-
Iran yalaani madai ya viongozi wa Ulaya na mawaziri wa fedha wa G7 dhidi yake
Apr 18, 2024 23:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekanusha madai ya viongozi wa nchi za Ulaya na mawaziri wa fedha wa kundi la G7 pamoja na matamshi ya baadhi ya wakuu wa Marekani na kusema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitosita hata mara moja kujihami na kulinda maslahi yake ya kitaifa.
-
Ustawi wa biashara ya nje yenye mlingano chini ya uongozi wa serikali ya 13 ya Iran
Apr 18, 2024 23:14Kituo cha Takwimu cha Kamisheni ya Ulaya kimetangaza kuwa Katika mwezi wa kwanza wa mwaka huu wa 2024, uagizaji wa bidhaa wa Ugiriki kutoka Iran uliongezeka mara 3 na Uholanzi mara 2, nayo mauzo ya Uhispania kwa Iran yakaongezeka kwa asilimia 62 na Italia kwa asilimia 13.
-
Gharibabadi: Nchi za Magharibi ziache sera za kinafiki na ubaguzi kuhusiana na ugaidi
Apr 18, 2024 10:05Katibu wa Baraza Kuu la Haki za Kibinadamu la Iran amesema kuwa, Marekani na nchi za Magharibi kwa ujumla zinapaswa kuachana na siasa zao za kindumakuwili na ubaguzi kuhusiana na ugaidi.
-
SEPAH: Vitisho vya Israel dhidi ya Iran si vipya na Tehran muda wote iko tayari kujibu mashambulizi ya adui
Apr 18, 2024 10:00Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya nchini Iran SEPAH amesema kuwa, vitisho vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran haviwezi kuifanya Jamhuri ya Kiislamu kubadilisha sera na siasa zake kuhusu kustafidi kwa njia ya amani na teknolojia ya nyuklia.
-
Kukiri Pentagon kuhusu uwezo wa kijeshi wa Iran katika kuujibu utawala wa Kizayuni
Apr 18, 2024 08:49Patrick Ryder Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) amekiri juu ya nguvu za kijeshi za Iran katika kutoa jibu la kijeshi kwa utawala wa Israel.