-
Waziri wa Ulinzi: Iran iko tayari kuisaidia Syria kuimarisha nguvu zake za kiulinzi na za kuzuia mashambulio
Mar 17, 2024 02:28Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Mohammad Reza Ashtiani amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kutumia uwezo wake wote kuisaidia Syria katika kuimarisha ulinzi na uwezo wake wa kuzuia hujuma za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Iran yaipongeza Afrika Kusini kwa kuishtaki Israel katika mahakama ya ICJ
Mar 16, 2024 23:25Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameipongeza na kuishukuru Afrika Kusini kwa uamuzi wake wa kihistoria wa kuwasilisha kesi dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kuhusu jinai za mauaji ya kimbari zinazotekelezwa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Vikwazo vya upande mmoja; ukiukaji wa haki za binadamu
Mar 16, 2024 22:40Balozi na Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika makao ya Umoja wa Mataifa barani Ulaya huko Geneva Uswisi amesema kuwa leo hii madhara ya vikwazo haramu vya upande mmoja yamedhihirika wazi mbele ya walimwenu ambapo vimefanya hali ya migogoro ya kibinadamu kuwa mbaya zaidi sambamba na kuchochea ukiukwaji wa haki za kimsingi za binadamu.
-
Kan'ani: Ndoto za kuigawa vipande vipande Iran zitazikwa kwenye kaburi la sahau
Mar 16, 2024 07:53Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amejibu matamshi ya kijuba na ya kipuuza na kiongozi mmoja wa utawala wa Kizayuni wa Israel na kusema kuwa, ndoto za kuigawa vipandevipande Iran zitazikwa kwenye kaburi la sahau kama zilivyozikwa njozi nyingine za maadui.
-
Iran yatiwa wasiwasi na kushtadi kampeni za chuki dhidi ya Uislamu
Mar 16, 2024 03:52Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema Jamhuri ya Kiislamu inatiwa wasiwasi na hatua ya kupanuka mtandao wa kampeni za chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu duniani.
-
Marekani ndiye mshutumiwa nambari moja wa kuvunja haki za binadamu
Mar 15, 2024 22:53Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Marekani ndiye mshutumiwa nambari moja wa uvunjaji wa haki za binadamu hasa hivi sasa ambao unausheheneza silaha za mauaji ya kimbari utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Hatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran: Hali ya Gaza inamfanya kila mwanadamu alie machozi ya damu
Mar 15, 2024 10:01Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amelitaja suala la Gaza na Palestina kuwa ndiyo kadhia ya kwanza ya Ulimwengu wa Kiislamu.
-
Amir-Abdollahian: Adui Mzayuni hajaweza kufikia malengo yake katika vita vya Ghaza
Mar 15, 2024 04:27Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian amesema, adui Mzayuni hajaweza kufikia hata moja kati ya malengo aliyoyatangaza kuhusiana na vita vya Ghaza. Amir-Abdollahian ameyasema hayo katika salamu zake kwa viongozi wa makundi ya muqawama na wananchi wenye istikama na subira wa Lebanon na Palestina ambapo sambamba na kuenzi kumbukumbu za mashahidi wa Muqawama ametoa mkono wa kheri na baraka pia kwa mnasaba wa kuandama mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Iran yalaani kupewa uanachama Israel kwenye Baraza la Haki za Binadamu
Mar 14, 2024 23:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, utawala wa Kizayuni ambao unafanya mauaji ya kimbari dhidi ya watoto wadogo huko Palestina haustahiki kabisa kuwa mwanachama wa mashirika ya haki za binadamu na ya misaada duniani likiwemo baraza la kupigania haki za wanawake la Umoja wa Mataifa.
-
Iran yalaani vikwazo vya upande mmoja vya Magharibi dhidi ya mataifa huru
Mar 14, 2024 10:43Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika makao makuu ya Umoja wa Umoja wa Mataifa mjini Geneva amesema: Vikwazo vya upande mmoja vimepelekea kukithiri machafuko ya kibinadamu kote duniani.