-
Mizizi ya ukoloni katika mzozo wa India na Pakistan
May 11, 2025 22:28Mzozo wa India na Pakistan ni moja ya migogoro sugu na ya muda mrefu zaidi katika eneo la Asia Kusini.
-
Jinamizi la kukwama safari za ndege laendelea kuitesa Israel
May 11, 2025 08:46Mashambulizi ya Jeshi la Yemen dhidi ya viwanja vya ndege vya utawala wa Kizayuni hususan Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion wa Tel Aviv yanaendelea kuisababishia jinamizi Israel hususan baada ya Yemen kuapa kuvigeuza Jahannam viwanja hivyo vya utawala wa Kizayuni mpaka ukomeshe jinai zake huko Ghaza.
-
Foreign Affairs: Dola bilioni 2 za Marekani zimeshindwa kuipigisha magoti Yemen
May 11, 2025 08:37Jarida la makala za uchaguzi la Foreign Affairs limesisitiza kuwa licha ya rais wa Marekani, Donald Trump kudai kuwa Ansarullah ya Yemen imesalimu amri, lakini harakati hiyo haijaathiriwa na mashambulizi ya Marekani yaliyoitia hasara ya dola bilioni mbili nchi hiyo, na wanamapambano wa Yemen wanaendelea na mashambulizi yao dhidi ya Israel.
-
Aragchi: Haikubaliki kuwa na wasiwasi kuhusu mpango wa nyuklia wa amani wa Iran huku Israel ikiwa na silaha za nyuklia
May 11, 2025 05:46Iran imekosoa undumakuwili wa jamii ya kimataifa kuhusu silaha za nyuklia, na kusema “haikubaliki” kwa madola ya Magharibi kudai kuwa na wasiwasi kuhusu mpango wa nishati ya nyuklia wa amani wa Iran huku yakifumbia macho silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Kufurushwa au Kufa: UNICEF yakosoa mpango wa Israel wa misaada Gaza
May 11, 2025 05:42Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limekosoa vikali mpango tata wa misaada kwa Ukanda wa Gaza unaoungwa mkono na Marekani na Israel, likionya kuwa unaweza kulazimisha familia kuchagua kati ya "kuondoshwa makwao au kufa."
-
Nakba Nyingine: UN yaonya kuhusu kuhamishwa kwa nguvu kwa Wapalestina
May 11, 2025 00:58Kamati Maalumu ya Umoja wa Mataifa imeonya kwamba dunia inaweza kuwa inashuhudia “Nakba nyingine” huku utawala wa Israel ukiendelea na mpango wake wa kuwaondoa kwa nguvu maelfu ya Wapalestina katika ardhi yao kwenye vita vyake vya muda mrefu vya mauaji ya kimbari dhidi ya Ukanda wa Gaza.
-
India na Pakistan zaonyesha nia ya kupunguza mzozo kwa masharti
May 10, 2025 08:51India na Pakistan leo Jumamosi zimeonyesha nia yao ya kumaliza mzozo wao wa kijeshi iwapo pande zote mbili zitaheshimu uamuzi huo. Hata hivyo, majeshi ya pande hizo mbilii yameendelea kushambuliana kwa silaha za aina mbaliimbali.
-
Ndege za kivita za Israel zashambulia ghala la chakula la UNRWA huko Jabalia + Video
May 10, 2025 03:27Shirika la Habari la Palestina limetangaza kuwa, ndege za kivita za Israel zimeshambulia ghala la chakula la UNRWA katika kambi ya Jabalia ya kaskazini mwa Ghaza.
-
Si gereza Israel ni makaburi, ukitoka hai ndio ushangae
May 10, 2025 03:26Askari mmoja wa akiba wa jeshi la Israel ambaye wakati fulani alikuweko kwenye jela ya kutisha ya Israel ya Sde Teiman katika Jangwa la Negev amefichua taarifa za kutisha na kuogofya mno kuhusu jinai wanazofanyiwa Wapalestina kwenye gereza hilo.
-
Israel yatumia njaa kama silaha ya vita huku Mabakeri yote Gaza yakifungwa
May 10, 2025 00:58Utawala haramu wa Israel unaendelea kutumia njaa kama silaha ya vita huku taarifa zikisema unga wa ngano umemalizika kabisa katika Ukanda wa Gaza, na kusababisha kufungwa kwa mabakeri yote.