-
Mahujaji wa Nyumba Tukufu ya Allah wasimama Arafa
Jun 05, 2025 09:30Mahujaji wa Nyumba Tukufu ya Mwenyezi Mungu leo wamesimama katika uwanja wa Arafa kisimamo hicho kikiashiria kilele cha ibada tukufu ya Hijja.
-
Mufti wa Oman ataka mataifa ya dunia kujifunza kutoka kwa Yemen
Jun 05, 2025 09:23Mufti Mkuu Oman, Sheikh Ahmed bin Hamad Al-Khalili, amesisitiza kuwa, leo hii majeshi ya madola dhalimu na ya kibeberu duniani yameinamisha vichwa vyao mbele ya Yemen na ameyataka mataifa yanayotaka kuwa huru duniani, kuiga mfano wa Yemen katika kukabiliana na maadui wa mataifa yao.
-
Hamas: Veto ya Marekani ni kuipa idhini Israel kufanya uhalifu zaidi
Jun 05, 2025 09:11Harakati za HAMAS na Jihadul Islami za Palestina zimetoa taarifa za kulaani vikali hatua ya Marekani ya kutumia kura ya turufu katika Baraza la Usalama na kusisitiza kuwa hatua hiyo ni kuzidi kuipa idhini Israel ifanye jinai kubwa zaidi.
-
Iran: Tutaendelea kuiunga mkono Lebanon kwa hali na mali
Jun 05, 2025 03:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesisitiza utayarifu wa Jamhuri ya Kiislamu kuimarisha ushirikiano na Lebanon, alipokutana na Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah, Sheikh Naim Qassem mjini Beirut.
-
Umoja wa Mataifa: Kuwanyima Wapalestina kupata chakula ni uhalifu wa kivita
Jun 04, 2025 09:33Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu, akikosoa jinsi misaada inavyosambazwa katika Ukanda wa Gaza, ametangaza kuwa, kuwanyima raia kupata chakula huko Gaza kunaweza kuwa uhalifu wa kivita.
-
Kwa nini mashinikizo dhidi ya Netanyahu hayafanyi kazi?
Jun 04, 2025 07:32Mauaji ya Wapalestina wanaoishi Gaza yanayofanywa na utawala wa Kizayuni yangali yanaendelea, huku nchi na jumuiya mbalimbali za kimataifa zikitoa wito wa kukomeshwa mauaji hayo mara moja.
-
Jordan yawashutumu walowezi wa Israel kuingia kwa nguvu Al-Aqsa
Jun 03, 2025 23:17Wizara ya Mambo ya Nje na Masuala ya Wageni ya Jordan imelaani vikali vitendo vya mara kwa mara vya walowezi wa Kizayuni kuvamia Msikiti wa Al-Aqsa.
-
Israel imeua Wapalestina zaidi ya 54,500 huko Gaza tangu Oktoba 2023
Jun 03, 2025 23:03Idadi ya vifo vya Wapalestina katika vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendelea Gaza, ambavyo vilianza Oktoba 7 2023, sasa imepindukia 54,500. Aghalabu ya waliouawa ni wanawake na watoto. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Afya ya Ukanda huo iliyotolewa Jumanne.
-
WFP: Watu milioni mbili wanataabika na njaa Gaza
Jun 03, 2025 07:40Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetangaza kuwa zaidi ya watu milioni mbili katika Ukanda wa Gaza wanakabiliwa na njaa kali, huku wengi wao wakikaribia kukumbwa na ukame na ukata wa ajabu.
-
Jeshi la Israel lapata kipigo kingine kikubwa kutoka kwa HAMAS
Jun 03, 2025 03:34Wanajeshi vamizi wa Israel wameingia kwenye mtego uliotegwa na Brigedi za Izzuddin al Qassam, Tawi la Kijeshi la HAMAS huko Jabalia, kaskazini mwa Ghaza na wamepoteza wanajeshi kadhaa.