-
Wazayuni wamefanya mashambulizi 24,000 katika Ukingo wa Magharibi
Jan 06, 2026 23:26Ripoti ya kila mwaka ya shirika moja la Palestina imefichua kuwa, katika kipindi cha mwaka uliopita wa 2025, Wazayuni wamefanya karibu mashambulizi 24,000 katika eneo la Ukingo wa Magharibi la Mto Jordan huko Palestina.
-
Israel yafanya mashambulizi makubwa ya anga dhidi ya Lebanon
Jan 06, 2026 08:40Israel imefanya mfululizo wa mashambulizi ya anga katika maeneo yote ya kusini na mashariki mwa Lebanon, ikiendelea kukanyaga makubaliano ya kusitisha mapigano ambayo lengo lake ni kukomesha uchokozi wa Israeli dhidi ya uhuru wa kujitawala nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Kuondoka vikosi vya kigeni, suluhisho pekee la mgogoro wa Yemen
Jan 06, 2026 08:39Kiongozi mmoja mwandamizi wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa, kuendelea kuwepo wanajeshi vamizi ndani ya ardhi ya Yemen ni tatizo kuu la mgogoro wa nchi hiyo akisisitiza kwamba upatanishi wowote kutoka nchi jirani hausaidii, kwani wao wenyewe hao wapatanishi ndio wahusika wakuu wa mgogoro wa Yemen.
-
Hamas imerejesha nafasi yake kama mtawala wa Ukanda wa Ghaza
Jan 05, 2026 23:50Shirika la habari la Tasnim limevinukuu vyombo vya habari vya Israel vikitangaza kuwa, Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imerejesha udhibiti wake kama mtawala mwenye nguvu kwenye Ukanda wa Ghaza.
-
Saudia yaendelea kushambulia maeneo ya mamluki wa Imarati nchini Yemen
Jan 05, 2026 23:50Ndege za kivita za Saudi Arabia zimeendelea kufanya mashambulizi dhidi ya maeneo ya mamluki wa Imarati yakiwemo makao makuu ya mamluki hao huko mashariki mwa Yemen.
-
Hamas yailaani vikali Israel kwa kuendelea kukiuka usitishaji vita Gaza
Jan 05, 2026 04:28Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeilaani vikali Israel kwa kuendelea kukiuka makubaliano ya usitishaji mapigano katika Ukanda wa Gaza na kutahadharisha kuwa hatua kama hizo zinatishia kudhoofisha makubaliano hayo yanayolegalega.
-
Viongozi wa Iraq: Qassem Soleimani alikuwa na mchango mkubwa katika kuliangamiza kundi la Daesh
Jan 04, 2026 23:15Viongozi wa Iraq wamesisitiza mchango muhimu wa shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani katika kuliangamiza kundi la kigaidi la Daesh kulinda mafanikio ya ushindi huo.
-
Umoja wa Maulamaa wa Muqawama wakosoa ulimwengu wa Kiislamu kwa uzembe kuhusu hali ya Gaza
Jan 04, 2026 23:14Mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Maulamaa wa Muqawama amekosoa vikali uzembe wa Ulimwengu wa Kiislamu kuhusiana na hali ya Ukanda wa Gaza.
-
Muqawama: Mashambulizi ya Venezuela yameanika dhati ya Marekani
Jan 04, 2026 08:42Makundi ya Muqawama katika eneo la Asia Magharibi sanjari na kulaani kile yalichokiita ugaidi wa kiserikali wa Marekani dhidi ya Venezuela, yamesema mashambulizi na utekaji nyara wa Rais Nicolas Maduro wa Venezuela kwa mara nyingine tena umeanika dhati na hulka halisi ya Marekani.
-
Hizbullah: Iran haijataka chochote kwetu mkabala wa kutusaidia, kutuunga mkono
Jan 04, 2026 07:36Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Sheikh Naim Qassem amepongeza ustadi wa kijeshi wa aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Luteni Jenerali Qassem Soleimani na kuongeza kuwa, Iran haijataka chochote kutoka kwa harakati hiyo ya Muqawama mkabala wa uungaji mkono wake kwake.