Polisi ya Zimbabwe yakabiliana tena na wapinzani wa serikali ya Mugabe
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i14021-polisi_ya_zimbabwe_yakabiliana_tena_na_wapinzani_wa_serikali_ya_mugabe
Kwa mara nyingine tena polisi nchini Zimbabwe imekabiliana na waandamanaji dhidi ya serikali katika mji mkuu wa nchi hiyo, Harare.
(last modified 2026-05-02T17:46:50+00:00 )
Aug 26, 2016 12:07 UTC
  • Polisi ya Zimbabwe yakabiliana tena na wapinzani wa  serikali ya Mugabe

Kwa mara nyingine tena polisi nchini Zimbabwe imekabiliana na waandamanaji dhidi ya serikali katika mji mkuu wa nchi hiyo, Harare.

Makabiliano hayo yamejiri leo Ijumaa wakati wapinzani walipoingia mitaani wakitaka kufanyika marekebisho katika mfumo wa uchaguzi nchini. Washiriki katika maandamano hayo wamemtaka Rais Robert Mugabe kufanya marekebisho ya sheria za uchaguzi kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2018 sanjari na kuondoka kwake madarakani.

Polisi ya Zimbabwe wakikabiliana na waandamanaji 

Waandamanaji pia wamemtuhumu Rais Mugabe kuwa anaongoza nchi hiyo kwa mfumo wa udikteta na wamemtaka aondoke mara moja madarakani.

Katika miezi ya hivi karibuni polisi ya nchi hiyo imekuwa ikikabiliana na maandamano ya kulalamikia ukosefu wa ajira na ufisadi nchini Zimbabwe, na inatumia nguvu kuzima malalamiko hayo ya wananchi.

Polisi wa Zimbabwe wakikabiliana na waandamanaji 

Hivi karibuni pia askari polisi wa Zimbabwe walitumia mabomu ya kutoa machozi na mipira ya maji kuwatawanya vijana wa chama cha upinzani cha MDC waliokuwa wakiandamana kupinga ukatili unaofanywa na maafisa wa usalama.