Askari wa kimataifa watuhumiwa kufanya uhalifu DRC
Kamati ya nidhamu ya askari wa Umoja wa Mataifa wanaolinda amani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesema kuwa, askari wa umoja huo wanatumuhimiwa kufanya vitendo visivyo vya kimaadili mwaka 2016 nchini Kongo.
Adama Ndao, mratibu wa kamati hiyo amesema, mwaka 2016 kuliripotiwa kesi 15 za vitendo vya uvunjifu wa maadili vinavyodaiwa kufanywa na askari wa kimataifa wa kulinda amani huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Aidha mratibu huyo wa kamati ya nidhamu ya askari wa Umoja wa Mataifa wanaolinda amani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametaka wahojiwe raia, wanajeshi, serikali na askari wa kulindi amani wa Umoja wa Mataifa kuhusu suala hilo.
Mwezi Machi 2016, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilitoa azimio la kuwabana zaidi askari wa kulinda amani ambao wanafanya uhalifu na vitendo visivyo vya kimaadili katika nchi yoyote ile ulimwenguni.
Katika ripoti yake ya hivi karibuni Umoja wa Mataifa ulisema kuwa, mwaka uliopita wa 2016, vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu viliongezeka kwa asilimia 30 ikilinganishwa na mwaka wa kabla yake yaaani wa 2015 huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.