Jeshi la Kongo lakomboa baadhi ya maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo
Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limeyakomboa baadhi ya maeneo ya jimbo la Fizi mkoani Kivu ya Kusini mashariki mwa nchi hiyo kutoka mikononi mwa waasi wa Mai-Mai.
Safari Gustave Bwange, kamanda wa oparesheni ya "Sokola 2" na 3" ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika mkoa wa Kivu ya Kusini amesema kuwa, jeshi la nchi hiyo limewafurusha waasi wa Mai-Mai katika maeneo ya Nyange na Ngalula katika eneo la Fizi.
Gustave Bwange ameongeza kuwa, wakazi wa maeneo hayo ya mashariki mwa Kongo wameyakimbia makazi yao kufuatia mapigano kati ya vikosi vya serikali na waasi. Kamanda wa jeshi la Kongo amesisitiza kuwa, wafanyabishara wa miji ya kandokando na mkoa wa Kivu ya Kusini wanakabiliwa na hali ngumu katika shughuli zao kutokana na mapigano hayo.
Waasi wa Mai-Mai Jumamosi iliyopita waliyavamia na kuyakalia baadhi ya maeneo ya jimbo la Fizi baada ya kukabiliana na wanajeshi wa serikali.