-
Kuchukuliwa hatua ndogo katika vita vya Ghaza ni muhimu lakini hakutoshi
Oct 22, 2023 22:52Licha ya kwamba mashambulizi ya mauaji ya umati ya utawala wa Kizayuni dhidi ya wakazi zaidi ya milioni mbili na laki tatu wa Ukanda wa Ghaza yameingia katika wiki ya tatu ambapo yamesababisha majeruhi na kuawa shahidi Wapalestina zaidi ya elfu 16 na zaidi ya wakazi wa Ghaza milioni moja kuhama makazi yao, lakini kuchukuliwa hatua kadhaa, japo ni madogo, huenda kukaandaa uwanja wa kudhibitiwa mapigano na kupunguzwa machungu ya wananchi wa Palestina.
-
Kimya cha Baraza la Usalama kuhusu kuhamishwa zaidi ya asilimia 60 ya wakazi wa Ghaza
Oct 22, 2023 07:55Katika hali ambayo kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa, zaidi ya asilimia 60 ya wakazi wa Ukanda wa Ghaza wamehama makazi yao kutokana na jinai za utawala wa Kizayuni, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa bado limekaa kimya kuhusu suala hilo huku madola ya Magharibi ya baraza hilo yakichochea na kuunga mkono jinai hizo za Tel Aviv.
-
Kuendelea radiamali ya wananchi na nchi za Kiislamu kwa jinai za Israel dhidi ya Wapalestina
Oct 22, 2023 04:19Jinai za utawala wa kibaguzi wa Israel katika Ukanda wa Gaza zimeendelea kulaaniwa na tawala na mataifa mbalimbali ya duniani hususan madola na nchi za Kiislamu.
-
Vipimo viwili tofauti vya Ulaya kuhusu uhuru wa kujieleza; vitisho na adhabu kwa waungaji mkono wa Palestina
Oct 21, 2023 23:07Matukio ya hivi karibuni huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu na Israel hasa baada ya mashambulizi ya Kimbunga cha Al-Aqsa na jibu la kinyama la utawala wa Kizayuni, hasa mashambulizi ya kikatili ya utawala huo dhidi ya wanawake na watoto wa Ukanda wa Ghaza, yameibua radiamali kali ya jamii ya kimataifa dhidi ya utawala huo.
-
Ushirikiano wa Korea Kaskazini na Russia dhidi ya Marekani
Oct 21, 2023 07:58Katika mazungumzo yake na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, Sergei Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, wamejadiliana kuhusu uhusiano wa pande mbili na ushirikiano wao wa hivi sasa na kusisitiza juu ya makubaliano yao ya kutatua kidiplomasia masuala yenye utata katika Peninsula ya Korea.
-
Uungaji mkono wa pamoja wa Serikali na wananchi wa mataifa ya Kiislamu kwa Palestina
Oct 21, 2023 02:46Moja ya matunda muhimu yaliyopatikana kutokana na jinai za kinyama na za kutisha zilizofanywa, na zinazoendelea kufanywa na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina ni kujitokeza msimamo na mwafaka wa pamoja wa Serikali na wananchi wa mataifa ya Kiislamu katika kuiunga mkono Palestina.
-
Hatimaye Netanyahu amdhibiti Biden
Oct 20, 2023 22:54Biden ambaye awali alijiepusha kumwalika Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala wa kibaguzi wa Israel katika Ikulu ya White House, ameshawishika kukubali hila za Netanyahu, ambapo amesimamisha shughuli zake zote huko Marekani na kuamua kumtembelea katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu katika kilele cha uzee wake.
-
Holocaust ya karne mara hii yatekelezwa Gaza
Oct 20, 2023 09:00Wakati dunia ingali katika mshangao wa kushambuliwa kwa mabomu hospitali iliyojaa Wapalestina waliojeruhiwa na jeshi la utawala ghasibu wa Israel, mashambulizi makali ya anga na makombora ya utawala huo yangali yanaendelea dhidi ya Ukanda mzima wa Ghaza kwa wiki ya pili mfululizo.
-
Wasiwasi wa kimataifa kuhusu mgogoro wa kibinadamu Ukanda wa Ghaza
Oct 19, 2023 23:07Shambulio la utawala wa Kizayuni katika hospitali huko katika Ukanda wa Ghaza limelaaniwa na pande mbalimbali kimataifa.
-
Kikao kisichokuwa na natija cha Baraza la Usalama: Marekani yapinga usitishaji mapigano Gaza
Oct 19, 2023 07:20Jumatano, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilikataa tena azimio la kusitisha mapigano huko Gaza kufuatia upinzani wa Marekani. Marekani ilipinga azimio lililopendekezwa kwa Baraza la Usalama na Brazil, lililotaka kusitishwa mapigano ili kufikishwa misaada ya kibinadamu Ghaza.