-
Bab al-Mandab, mstari mpya wa kuzuia hujuma na kuimarisha uwiano wa "Umoja wa Medani"
Jun 08, 2026 12:10Msemaji wa Jeshi la Yemen ametangaza kwamba kuanzia sasa jeshi hilo limeanza kutekeleza amri ya kupiga marufuku kikamilifu meli zote za utawala haramu wa Israel kupita katika maji ya Bahari ya Shamu au kwa Kiingereza Red Sea na kwamba kuanzia wakati wa kutangazwa marufuku hiyo na kuendelea urambazaji wa baharini wa Israel katika Bahari Nyekundu utakuwa shabaha halali ya jeshi la wanajeshi wa Yemen.
-
Jibu kali la makombora la Iran kwa ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita na jinai za Israel nchini Lebanon
Jun 08, 2026 08:03Iikiwa ni katika kunufaika na haki yake ya kujilinda na kujibu ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita na jinai za kinyama zinazofanywa na utawala dhalimu wa Israel dhidi ya watu wa Lebanon, vikosi vya jeshi la Iran Jumapili usiku vilitoa jibu kali la makombora katika maeneo ya utawala huo katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu. Maeneo yaliyolengwa katika shambulio hilo kubwa la makombora kimsingi ni ya kijeshi na kistratijia ya utawala wa Israel.
-
Kwa nini washirika wa Washington sasa wana wasiwasi kuhusu uwepo wa kambi za Marekani katika ardhi zao?
Jun 07, 2026 11:10Kwa mujibu wa jarida la Foreign Affairs la nchini Marekani, vita na Iran vinaweza kutoa changamoto kubwa kwa jeshi la Marekani na hasa kuhusu hatari ya kushambuliwa kambi zake za kijeshi katika siku zijazo.
-
Kwa nini Ulaya inataka kufafanua upya uhusiano wake na China?
Jun 06, 2026 12:48Ufaransa na nchi nyingine nne za Ulaya, katika mkesha wa mkutano wa kimkakati wa Kamisheni ya Ulaya kuhusu China, zilitoa wito wa kuundwa vyombo vipya vya kutetea biashara ili kulinda viwanda vya Ulaya na kukabiliana na ushindani kutoka kwa makampuni yanayoungwa mkono na serikali ya Beijing.
-
Je, Israel inafuatilia malengo gani katika kuzidisha vita nchini Lebanon?
Jun 03, 2026 12:13Utawala wa Kizayuni unaendelea kushambulia Lebanon ambapo katika siku za hivi karibuni ulikuwa umetishia kuushambulia mtaa wa Dhahiyah kusini mwa Beirut na kutaka watu wahame kutoka eneo hilo. Swali muhimu ni je, kwa nini utawala wa Kizayuni unataka kushadidisha mgogoro na vita nchini Lebanon?
-
Hormuz, vita na ukweli ambao Washington haikuwa na budi ila kuukubali
Jun 03, 2026 07:08Katika hali ambayo sera ya "mashinikizo ya juu zaidi" na chaguo la kijeshi la Trump vilipaswa kuilazimisha Iran ilegeze msimamo na kurudi nyuma, lakini matukio ya karibuni yameonyesha kuwa Washington inatafuta njia ya kujiondoa kwa heshima katika mgogoro ambao imejianzishia yenyewe.
-
Lengo la Marekani kutokana na siasa zake zenye mgongano katika eneo la Asia-Pasifiki
Jun 02, 2026 10:04Waziri wa Vita wa Marekani amesema katika mkutano wa Shangri-La huko Singapore kwamba Washington inatarajia washirika wake wa Asia waongeze matumizi yao ya kijeshi na ulinzi hadi asilimia 3.5 ya Pato lao la Taifa.
-
Je, ni vipi Ulaya imekuwa mshirika wa jinai za utawala wa Kizayuni?
Jun 01, 2026 09:59Jürgen Todenhofer, mwanasiasa na mjumbe wa zamani wa bunge la Ujerumani, amesema: "Umoja wa Ulaya na serikali ya Ujerumani zinahusika moja kwa moja katika maangamizi makubwa ya watu wa Palestina."
-
Kwa nini Trump anatapatapa kati ya vitisho na makubaliano?
May 31, 2026 13:18CNN imesema katika ripoti kwamba: "Serikali ya Marekani huchanganyikiwa linapokuja suala la nyuklia la Iran." Katika kipindi cha wiki kadhaa zilizopita, Rais Donald Trump wa Marekani amebadilisha misimamo yake mara kadhaa kuhusu hatima ya hifadhi ya urani iliyorutubishwa ya Iran.
-
Kwa nini utawala wa Kizayuni unasisitiza kuendeleza vita huko Lebanon?
May 30, 2026 07:00Moja ya vikwazo muhimu katika mazungumzo ya Iran na Marekani ni sisitizo la utawala wa Kizayuni wa Israel la kuondolewa medani ya vita vya Lebanon kwenye mazungumzo hayo na kuendeleza vita dhidi ya harakati ya Hizbullah. Hii ni katika hali ambayo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa moja ya masharti muhimu ya kufikiwa mapatano na Marekani ni kusimamishwa kikamilifu vita katika ngome zote za mhimili wa muqawama na hasa nchini Lebanon.