May 04, 2024 02:30
Sambamba na kuendelea kupanuka maandamano ya wanafunzi wa Marekani na juhudi za Mahakama ya ICJ na ICC za kutoa waranti wa kukamatwa viongozi wa utawala wa kibaguzi wa Israel kutokana na jinai zao huko Gaza, Shirika la Haki za Binadamu la Euro-Mediterranean limetoa ripoti mpya na ya kutisha inayoweza kuzidisha hasira za wanafunzi hao na wakati huo huo kuongeza ushahidi mpya katika jinai zinazofanywa na utawala huo dhidi ya Wapalestina.