Utumiaji mbaya wa silaha Marekani wasababisha vifo vya watu wawili
https://parstoday.ir/sw/news/daily_news-i130104-utumiaji_mbaya_wa_silaha_marekani_wasababisha_vifo_vya_watu_wawili
Shule moja katika mji wa Minneapolis, ulioko katika jimbo la Minnesota, siku ya Jumatano, ilishuhudia maafa mengine yaliyotokana na utumizi mbaya wa silaha zilizoko mikononi mwa raia.
(last modified 2025-08-28T08:07:51+00:00 )
Aug 28, 2025 08:05 UTC
  • Utumiaji mbaya wa silaha Marekani wasababisha vifo vya watu wawili

Shule moja katika mji wa Minneapolis, ulioko katika jimbo la Minnesota, siku ya Jumatano, ilishuhudia maafa mengine yaliyotokana na utumizi mbaya wa silaha zilizoko mikononi mwa raia.

Wakati wanafunzi walipoingia shuleni, walishuhudia vurugu na ghasia za matumizi mabaya ya silaha, jambo lililosababisha vifo na kujeruhiwa watu kadhaa.

Afisa wa Idara ya Sheria ya Marekani amesema: 'Watu wawili waliuawa na wengine 20 kujeruhiwa kwa risasi katika shule ya Kikatoliki huko Minneapolis.'