COVID-19 nchini Iran: zaidi ya watu 215,000 wapata afueni
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i62123-covid_19_nchini_iran_zaidi_ya_watu_215_000_wapata_afueni
Msemaji wa Wizara ya Afya ya Iran ametangaza kuwa, hadi hivi sasa waathirika laki mbili na 15 elfu ugonjwa wa COVID-19 au corona humu nchini wamepata afueni na kuruhusiwa kurejea nyumbani kutoka mahospitalini na katika vituo vya afya.
(last modified 2026-08-21T06:20:04+00:00 )
Jul 10, 2020 20:12 UTC
  • COVID-19 nchini Iran: zaidi ya watu 215,000 wapata afueni

Msemaji wa Wizara ya Afya ya Iran ametangaza kuwa, hadi hivi sasa waathirika laki mbili na 15 elfu ugonjwa wa COVID-19 au corona humu nchini wamepata afueni na kuruhusiwa kurejea nyumbani kutoka mahospitalini na katika vituo vya afya.

Bi. Sima Sadat Lari, Msemaji wa Wizara ya Afya ya Iran ametangaza hayoIjumaa na kuongeza kuwa, wagonjwa wapya takribani 2000 wa COVID-19 wamegunduliwa nchini  Iran katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita kufikia jana adhuhuri. Amesema miongoni mwa kesi hizo mpya, wagonjwa 455 wamelazwa hospitalini na waliosaliwa wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa kurejea nyumbani.

Bi. Sadat Lari amongeza kuwa kwa ujumla watu walioambukizwa COVID-19 nchini Iran hadi jana mchana walikuwa  252,720. Halikadhalika aliongeza kuwa katika kipindi cha masaa 24 hadi jana adhuhuri, watu 142 walipoteza maisha kutokana na COVID-19 na hivyo kufanya idadi ya waliopoteza maisha Iran kutokana na ugonjwa huo kufika 12,447.

Idadi jumla ya walioambukizwa COVID-19 duniani hadi kufikia Ijumaa jioniilikuwa takriban milioni 12.3 na  na waliopoteza maisha hadi leo mchana ilikuwa ni zaidi ya watu zaidi ya 555,000 .

Tangazo la Wizara ya Afya ya Kenya kuhusu mojawapo ya njia kukabiliana na maambukizi ya COVID-19 au corona

Marekani inaongoza duniani kwa maambukizi na vifo vya COVID-19 ambapo hadi kufikia  Ijumaa jioni watu zaidi ya 3,165,058  walikuwa wameambukizwa COVID-19 na wengine wasiopungua 135,094 walikuwa wamepoteza maisha nchini Marekani pekee.