-
Baghaei: Jamii ya kimataifa ichukue hatua dhidi Israel
Dec 16, 2025 08:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani jinai zinazoendelea kufanywa na Israel huko Ghaza na mashambulizi yake dhidi ya Lebanon, na amezitaka nchi za ukanda huu na jamii ya kimataifa ichukue hatua kali za kukabiliana na tishio la mara kwa mara la utawala wa Kizayuni dhidi ya amani na utulivu wa eneo hili na dunia nzima kwa ujumla.
-
Iran yaitaka dunia izuie kuendelea mauaji ya Wapalestina Gaza
Dec 16, 2025 03:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, amelaani vikali kuendelea kwa mauaji ya halaiki ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, akiashiria mashambulizi ya mabomu yanayoendelea kufanywa na Wazayuni na kuzuiwa kwa misaada ya kibinadamu.
-
Mauzo ya chai ya Iran nje ya nchi yaongezeka kwa 48%
Dec 16, 2025 03:12Mkuu wa Shirika la Chai la Iran, Habib Jahansaz amesema mauzo ya chai ya Jamhuri ya Kiislamu nje ya nchi katika miezi minane ya kwanza ya mwaka huu wa kalenda ya Iran (ulioanza Machi 21) yameongezeka kwa asilimia 48, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana.
-
Iran: Madai ya kumiliki visiwa vya Ghuba ya Uajemi ni dhidi ya mamlaka ya kujitawala na ujirani mwema
Dec 15, 2025 23:58Iran imesema kuwa madai yoyote ya kumiliki visiwa vitatu vya Ghuba ya Uajemi yaani Tomb Kubwa, TombNdogo na Bu Musa ni ukiukaji wa kanuni za ujirani mwema na kutoheshimu mamla ya kujitawala ya nchi nyingine.
-
Mkutano wa Tehran; Ubunifu wa Iran kwa ajili ya mwafaka wa kikanda na uthabiti wa Afghanistan
Dec 15, 2025 11:29Mkutano wa wawakilishi maalum wa nchi jirani za Afghanistan pamoja na Russia umefanyika katika wizara ya mambo ya nje ya Iran, mjini Tehran.
-
Iran: IAEA haina haki ya kutaka kukagua vituo vilivyoshambuliwa
Dec 15, 2025 08:05Mkuu wa shirika la nyuklia la Iran amekosoa wito wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA wa kufanya ukaguzi mpya kwenye maeneo ya nyuklia yaliyoshambuliwa, akisisitiza kwamba taasisi hiyo ya UN haina itifaki zilizo wazi za kukagua maeneo ambayo yalishambuliwa na utawala wa Israel na Marekani.
-
IRGC: Maadui watakabiliwa na mwelekeo mpya wa uwezo wa Iran iwapo wataanzisha vita
Dec 15, 2025 07:30Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC Ali-Mohammad Naeini amesema kwamba ikiwa vita vitazuka, adui atakabiliwa na viwango vipya na vya hali ya juu vya nguvu ya kijeshi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Velayati: Iran inaiunga mkono Hizbullah ya Lebanon kwa dhati
Dec 15, 2025 03:26Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika Masuala ya Kimataifa amesema kuwa, Hizbullah ni moja ya nguzo muhimu zaidi za kambi ya Muqawama na ina jukumu la kimsingi katika kukabiliana na Uzayuni. Hivyo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, chini ya maagizo ya Kiongozi Muadhamu, itaendelea kuiunga mkono harakati hiyo ambayo iko mstari wa mbele katika Muqawama.
-
Kiwanda kikubwa cha nishati ya jua cha Iran kuzalisha umeme wa nyumba milioni 2.5
Dec 15, 2025 03:20Iran iko mbioni kukamilisha ujenzi wa kiwanda kikubwa cha nishati ya jua katika mkoa wa Isfahan wa katikati mwa Iran, mradi ambao unaotarajiwa kuzalisha umeme kwa karibu nyumba milioni 2.5 humu nchini.
-
Aragchi: Ushirikishwaji wa Afghanistan ni msingi wa uthabiti wa kudumu
Dec 14, 2025 22:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema uthabiti wa Afghanistan unategemea kuingizwa kwake kikamilifu katika mifumo ya kisiasa na kiuchumi ya kikanda, akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa majirani badala ya kutegemea nguvu za nje.