-
Marekani yarejesha vikwazo dhidi ya Ripota Maalumu wa UN kwa kufichua mauaji ya kimbari ya Israel
May 28, 2026 10:40Marekani imemuwekea tena vikwazo Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu kwa sababu tu ya kufichua mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
IRGC: Kituo cha uchokozi dhidi ya Bandar Abbas kimelengwa; uchokozi ukirudiwa, jibu litakuwa kali zaidi
May 28, 2026 10:06Idara ya Mahusiano wa Umma ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) imetangaza kuwa: Kituo cha anga cha Marekani kilichotumiwa kufanya uchokozi dhidi ya Bandar Abbas kusini mwa Iran, kimelengwa alfajiri ya leo Alkhamisi saa 10:50.
-
Kuanzia "Kujisalimisha Bila Masharti" hadi Kukubali Nguvu ya Iran; Kurudi Nyuma kwa Trump Chini ya Mashinikizo ya Ukweli wa Mambo
May 28, 2026 09:45Kushindwa Trump na Netanyahu katika kufikia malengo yao ya kuishambulia kijeshi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa mara ya pili katika kipindi cha miezi tisa, ni moja ya mada muhimu zinazojadiliwa na taasisi za utafiti, wananadharia mashuhuri na vyombo tajika vya habari.
-
Wanafunzi 16 wafariki dunia Kenya baada ya moto kuteketeza bweni Utumishi Girls Academy
May 28, 2026 09:39Wanafunzi 16 wameuawa baada ya moto kuteketeza bweni lao usiku wa kuamkia leo katika shule ya bweni huko Gilgil, (Utumishi Girls Academy) yapata kilomita 120 (maili 77) magharibi mwa mji mkuu wa Kenya, Nairobi, mamlaka imethibitisha.
-
IRGC: Iran imepata uwezo mpya wa kukabiliana na maadui
May 28, 2026 04:49Afisa mmoja mwandamizi wa kijeshi ameonya kwamba uchokozi wowote mpya wa kijeshi dhidi ya Iran utasababisha jibu la aina tofauti na lenye nguvu zaidi, “lisilofanana na chochote walichowahi kukiona hapo kabla.”
-
Al-Houthi: Umma wa Kiislamu unapaswa kujifunza kutokana na mapambano ya Iran dhidi ya Marekani na Israel
May 28, 2026 04:48Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa: Msimamo imara wa Iran unapaswa kuwa kichocheo cha kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
-
Ma'ariv: Maafisa 50 wa utawala unaotaka kujitenga Somaliland wamepewa nafunzo Israel
May 28, 2026 04:43Gazeti la Kiebrania la Ma'ariv limefichua kashfa mpya kuhusu uhusiano wa siri kati ya Tel Aviv na eneo linalotaka kujitenga huko kaskazini mwa Somalia, likiandika kwamba askari 50 wa "Somaliland" wamerejea Afrika baada ya kukamilisha kozi za mafunzo katika Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel).
-
HRW: Mamluki wa Colombia katika vita vya Sudan wanapewa mafunzo UAE
May 28, 2026 04:36Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limeripoti kwamba wapiganaji mamluki kutoka Colombia wanapewa mafunzo katika kambi za kijeshi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kisha wanapelekwa Sudan ili kuwasaidia waasi wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF).
-
Ayatullah Khatami: Trump ana jeni ya kusema uongo
May 27, 2026 15:17Imamu wa Swala ya Idul Adh'ha iliyofanyika mapema leo mjini Tehran amesema: "Maadui wanatamani taifa la Iran lichoke, lakini kwa neema ya Mungu, wataingia kaburi na matarajio hayo."
-
Kwa nini Trump anataka Pakistan iwe na uhusiano wa kawaida na utawala ghasibu wa Israel?
May 27, 2026 13:29Chanzo kimoja cha habari cha Pakistan kimeripoti kuhusu upinzani wa wazi wa Islamabad dhidi ya ombi la Rais Donald Trump wa Marekani la kuitaka nchi hiyo ijiunge na mchakato wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel, na kuongeza kuwa Islamabad inaiona hatua ya Washington kuwa jaribio la kutumia vibaya diplomasia ya "kusimamisha vita na Iran" ili kutoa mashinikizo katika kesi zisizohusiana.