Feb 27, 2024 12:43
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, imesema serikali ya Marekani inabeba dhima ya kifo cha mwanajeshi wa nchi hiyo aliyejichoma moto nje ya Ubalozi wa Israel huko Washington akipinga uungaji mkono wa serikali ya Rais Joe Biden kwa mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na Israel huko Ukanda wa Gaza.