Ripoti
  • Burundi yaadhimisha miaka 57 ya Uhuru + Sauti

    Burundi yaadhimisha miaka 57 ya Uhuru + Sauti

    Jul 01, 2019 11:36

    Leo Jumatano tarehe Mosi Julai 2019, Burundi imesherehekea mwaka wa 57 tangu ilipopata uhuru wake kutoka kwa mkoloni wa Ulaya, Ubelgiji. Rais Pierre Nkurunzinza ametumia fursa hiyo kutangaza hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kuondoa michango ya lazima kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2020. Hamida Issa na maelezo zaidi kutoka Bujumbura.

  • Mkuu wa Jeshi la Polisi la Tanzania atembelea eneo walipouliwa Watanzania + Sauti

    Mkuu wa Jeshi la Polisi la Tanzania atembelea eneo walipouliwa Watanzania + Sauti

    Jun 30, 2019 12:40

    Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania (IGP), Simon Sirro amesema imebainika kuwa waliowaua Watanzania 9 kwa kuwapiga risasi na wengine kushambuliwa kwa mapanga ambao ni watu wasiojulikana, walianza chokochoko hizo katika eneo la Kibiti mkoani Pwani baada ya kutimuliwa na na Jeshi la Polisi la Tanzania na wengine wakakimbilia nchi jirani ikiwemo Msumbiji. Maelezo zaidi yamo katika ripoti ya mwandishi wetu wa Dar es Salaam, Ammar Dachi.

  • Mbunge 'Jaguar' anyimwa dhamana nchini Kenya + Sauti

    Mbunge 'Jaguar' anyimwa dhamana nchini Kenya + Sauti

    Jun 28, 2019 12:43

    Mahakama nchini Kenya imemnyima dhamana, Mbunge wa eneobunge la Starehe jijini Nairobi Charles Njagua maarufu kwa jina la ‘Jaguar’ ambaye alikamatwa hivi karibuni na jeshi la polisi la nchi hiyo baada ya kutoa kauli ya kibaguzi dhidi ya Watanzania, Wachina na Waganda wanaoishi katika nchini hiyo mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mbunge huyo atasalia korokoroni hadi pale kesi yake itakaposikilizwa tena. Mwandishi wetu wa Mombasa, Kenya Seifullah Murtadha ana maelezo zaidi......

  • Matukio ya ulimwengu wa Kiislamu na Harith Subeit + Sauti

    Matukio ya ulimwengu wa Kiislamu na Harith Subeit + Sauti

    Jun 28, 2019 11:24

    Kama kawaida, wiki hii pia kuna matukio mengi ya Kiislamu yametokea katika ukanda mzima wa Afrika Mashariki. Mwandishi wetu wa Zanzibar, Harith Subeit ametukusanyia baadhi ya matukio hayo katika ripoti yake hii ya kila wiki...

  • Makumi ya watu waaga dunia kwenye mgodi Kongo DR + Sauti

    Makumi ya watu waaga dunia kwenye mgodi Kongo DR + Sauti

    Jun 28, 2019 11:01

    Makumi ya wachimba migodi wamefariki dunia baada ya kuporomokewa na udongo kwenye mgodi wa shaba nyekundu na kobalti huko kusini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

  • Kamati ya Mshikamano wa Wakenya na Wapalestina: Muamala ya Karne utagonga mwamba

    Kamati ya Mshikamano wa Wakenya na Wapalestina: Muamala ya Karne utagonga mwamba

    Jun 27, 2019 12:29

    Vuguvugu la mshikamano baina ya Wakenya na Wapelestina limekosoa vikali kimya cha jamii ya kimataifa mbele ya ukandamizaji wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina.

  • Polisi wawashikilia watuhumiwa 10 utekaji watu Rwanda + Sauti

    Polisi wawashikilia watuhumiwa 10 utekaji watu Rwanda + Sauti

    Jun 27, 2019 04:29

    Polisi mjini Kigali Rwanda inawashikilia watu kumi na saba wakiwemo Wanyarwanda 15 na Wakenya wawili kwa shutuma za kuwatapeli vijana zaidi ya elfu tatu wakiwaahidi ajira hewa za ujasiriamali. Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylivanus Karemera anaripoti zaidi...

  • SAUTI, Kazi ya ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme kwenye maporomoko ya Rusumo karibu itakamilika

    SAUTI, Kazi ya ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme kwenye maporomoko ya Rusumo karibu itakamilika

    Jun 24, 2019 13:36

    Nchi za Rwanda, Tanzania na Burundi zimetangaza kwamba kazi ya kuzalisha umeme kwenye maporomoko ya mto Rusumo iko mbioni kukamilika.

  • SAUTI, Mashirika matatu ya kujitegemea Burundi yalijia juu Shirika la Human Right Watch, yasema Burundi hali ni salama

    SAUTI, Mashirika matatu ya kujitegemea Burundi yalijia juu Shirika la Human Right Watch, yasema Burundi hali ni salama

    Jun 24, 2019 13:30

    Mashirika matatu yasiyokuwa ya kiserikali nchini Burundi yameipinga ripoti ya Shirika la Kutetea Haki za Binaadamu la Human Rights Watch iliyosema kuwa, bado kunaendelea hali ya ukandamizaji na ukiukaji mkubwa wa haki za binaadamu nchini humo.