-
Wacomoro waandamana kupinga jaribio la Rais wa nchi hiyo la kurefusha utawala wake
Oct 16, 2018 03:19Wananchi wa Comoro jana walifanya maandamano na kufunga barabara za mji wa Anjouan wakipinga jitihada zinazofanywa na Rais Azali Assoumani wa nchi hiyo za kutaka kurefusha kipindi cha uongozi wake na kukomesha mfumo wa kuongoza kwa zamu baina ya visiwa vitatu vikuu vinavyounda Jamhuri ya watu wa Comoro.
-
Ethiopia kuanza kuwapa Waafrika viza wakishawasili nchini humo
Oct 09, 2018 03:55Rais wa Ethiopia, Mulatu Teshome amesema nchi hiyo karibuni hivi itaanza kuwapa raia wote wa bara Afrika viza mara tu watakapowasili katika nchi hiyo.
-
Dukuduku la viongozi wa Afrika kuhusu kudhulumiwa bara hilo katika Umoja wa Mataifa
Oct 01, 2018 02:10Viongozi wengi wa Afrika wamelalamikia vikali utendaji na misimamo ya Umoja wa Mataifa kuhusu masuala na matatizo ya bara hilo na kulalamikia idadi ndogo ya wawakilishi wa Afrika wanaopewa nafasi kama wajumbe katika mashirika ya umoja huo.
-
Katumbi: Matokeo ya uchaguzi wa Kongo DR kuyumbisha uthabiti Afrika
Sep 23, 2018 04:28Moise Katumbi, mwanasiasa wa upinzani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambaye kwa sasa yuko uhamishoni nchini Ubelgiji ametadharisha kuwa, matokeo ya uchaguzi wa rais utakaofanyika nchini humo mwishoni mwa mwaka huenda yakavuruga amani na uthabiti sio tu katika nchi hiyo bali kote barani Afrika.
-
Trump azishauri nchi za Ulaya kujenga ukuta katika Jangwa la Sahara.
Sep 21, 2018 23:33Katika kuendeleza siasa zake zilizo dhidi ya uhamiaji na huku akiamini kwamba ujenzi wa kuta ndiyo njia bora zaidi ya kukabiliana na suala hilo, Rais Donald Trump wa Marekani amezishauri nchi za Ulaya kujenga ukuta katika Jangwa la Sahara ili kukabiliana na wimbi la wahajiri wa Kiafrika wanaohama nchi zao kuelekea nchi hizo.
-
Wabunge wa upinzani Zimbabwe wasusia hotuba ya Rais Mnangagwa
Sep 18, 2018 10:12Wabunge wa kambi ya upinzani nchini Zimbabwe mapema leo wameondoka bungeni na kususia hotuba ya Rais wa nchi hiyo, Emmerson Mnangagwa, ikiwa ni ishara ya hasira zao dhidi ya matokeo ya uchaguzi uliozusha utata wa rais ambayo yalimpa ushindi kiongozi wa chama tawala.
-
Qassemi: Uhusiano wa Iran na Afrika umesimama juu ya msingi wa kuheshimiana
Sep 18, 2018 10:12Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa uhusiano wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na nchi za Afrika daima umekuwa ukiheshimu mamlaka ya kitaifa ya kila nchi na kutilia mkazo suala la ustawi na ushirikiano.
-
Rais wa China alipatia bara la Afrika mabilioni ya dola; asema zisitumike katika miradi ya kifisadi
Sep 03, 2018 22:09Rais Xi Jinping wa China jana Jumatatu aliipatia Afrika kitita kingine cha dola bilioni 60 na kusema kuwa makampuni ya Kichina yatahimizwa kuwekeza kiasi kisichopungua chini ya dola bilioni 10 katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.
-
Watoto milioni tano wamefariki kutokana na vita na mapigano barani Afrika
Sep 01, 2018 09:37Watoto wapatao milioni tano wenye umri chini ya miaka mitano wamefariki dunia kutokana na vita na mapigano ya utumiaji silaha yaliyotokea katika kipindi cha miaka 20 iliyopita kwenye nchi za bara la Afrika.
-
Jitihada za FAO na AfDB za kupunguza umasikini kwa uwekezaji katika kilimo Afrika
Aug 29, 2018 00:04Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO zimekubaliana kuendeleza juhudi za pamoja za kuongeza uwekezaji katika sekta ya kilimo barani Afrika ili kukomesha njaa, na utapia mlo kwa lengo la kupanua wigo wa ustawi na maendeleo barani humo.