-
Mkuu wa Kituo cha Haki za Binadamu Bahrain akamatwa
Jun 13, 2016 07:50Katika kuendelea ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Bahrain, wanajeshi wa utawala wa Aal Khalifa wamemtia mbaroni Nabil Rajab, mkuu wa kituo cha haki za binadamu nchini humo.
-
Bahrain imeweka rekodi ya kuwa na wafungwa wengi katika Mashariki ya Kati
Jun 12, 2016 04:29Bahrain inaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wafungwa kati ya nchi za Mashariki ya Kati kulingana na idadi ya raia wote wa nchi hiyo.
-
UN: Kuongezewa adhabu ya kifungo Sheikh Salman ni ukandamizaji wa kisiasa
Jun 02, 2016 07:48Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya uhuru wa maoni na uhuru wa kujieleza amelaani vikali uamuzi wa mahakama ya rufaa ya Bahrain wa kuidhinisha hukumu iliyotolewa dhidi ya Sheikh Ali Salman, Katibu Mkuu wa Harakati ya Al-Wifaq na kuongeza adhabu hiyo ya kifungo hadi miaka tisa.
-
Radiamali ya Iran kufuatia kuongezewa adhabu ya kifungo Sheikh Ali Salman
Jun 01, 2016 07:31Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani hatua ya kumzidishia adhabu ya kifungo cha jela Sheikh Ali Salman, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kiislamu ya Kitaifa ya al Wifaq ya Bahrain.
-
Bahrain yasisitiza kuwanyonga wanaharakati 3 wa Kishia
Jun 01, 2016 07:02Mahakama ya Rufaa ya Bahrain imekataa kutengua hukumu ya kunyongwa wanaharakati watatu wa Kiislamu wa madhehebu ya Shia.
-
Umoja wa Mataifa Wakosoa Ukiukwaji wa Haki za Binadamu Bahrain na Saudia
May 31, 2016 07:39Sambamba na kutangazwa hukumu ya kidhalimu dhidi ya wanaharakati wa kisiasa wa Bahrain na Saudi Arabia, Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa limetoa ripoti na kuzituhumu tawala za nchi hizo mbili kuwa wakiukaji wakubwa wa haki za binadamu duniani.
-
Wananchi waandamana Bahrain kumuungamkono Sheikh Ali Salman
May 28, 2016 03:50Raia wa Bahrain kwa mara nyingine tena jana (Ijumaa) walifanya maandamano kuonyesha mshikamano wao kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kitaifa ya Kiislamu ya al Wifaq ya nchini humo, Sheikh Ali Salman.
-
Bahrain yakataa kumuachia huru mtoto wa miezi 17
May 24, 2016 16:21Serikali ya Bahrain imekataa ombi la mfungwa wa kisiasa Zainab al-Khawaja, kumuachia huru mwanawe wa miezi 17, kwa kuwa hali yake imedhoofu na hawezi tena kumshughulikia.
-
Hongo na ukandamizaji; silaha ya utawala wa Aal Khalifa ya kukabiliana na wapinzani Bahrain
May 22, 2016 16:19Ripoti kutoka Bahrain zinaeleza kuwa utawala wa kifalme wa ukoo wa Aal Khalifa unaendeleza siasa na sera zake za ukatili na ukandamizaji dhidi ya wapinzani na kushadidisha ukiukaji wa haki za binadamu.
-
Malkia wa Uingereza akosolewa kwa kushirikiana na Mfalme wa Bahrain
May 19, 2016 08:03Mashirika ya kutetea haki za binadamu ya Amnesty International na Human Rights Watch yamemjia juu Malkia Elizabeth II wa Uingereza kwa kumualika Mfalme wa Bahrain Hamad bin Isa Al-Khalifa katika sherehe za kuadhimisha miaka 90 ya kuzaliwa kwake, licha ya kufahamu dhulma na ukandamizaji unaofanywa na utawala wa Manama dhidi ya wananchi.