-
UN: Ebola inaua mtu mmoja kila baada ya nusu saa huko Congo DR
Aug 16, 2026 03:17Tom Fletcher, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Masuala ya Kibinadamu, ametangaza kwamba mlipuko wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo sasa unaua mtu mmoja kila baada ya nusu saa, akitoa wito kwa jamii ya kimataifa kuchukua hatua za haraka kupambana na mlipuko huo.
-
Mlipuko wa Ebola Kongo wapindukia maambukizi 4,000
Aug 08, 2026 02:42Idadi ya kesi za Ebola zilizothibitishwa hadi kufikia jana Ijumaa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zilikuwa zimepindukia 4,000 huku maeneo ya afya yaliyoathirika yakiongezeka.
-
Kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya Ebola DRC huku maambukizi yakienea
Aug 06, 2026 03:49Kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kimefunguliwa wiki hii na wadau wa Umoja wa Mataifa ikiwa ni hatua inayolenga kuimarisha mwitikio dhidi ya mlipuko wa sasa wa virusi vya Ebola aina ya Bundibugyo unaoendelea kuenea kwa kasi katika jimbo la Ituri, mashariki mwa taifa hilo.
-
WHO yaonya kuwa Uganda ingali iko katika hatari ya mripuko wa ebola
Jul 30, 2026 10:15Shirika la Afya Duniani, WHO leo limetoa indhari kwa Uganda kwamba ingali iko katika hatari kutokana na mripuko wa ugonjwa wa Ebola ulioenea katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Idadi ya vifo vya Ebola yazidi 1,000 Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Jul 24, 2026 02:40Idadi ya vifo kutokana na mlipuko wa sasa wa virusi vya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imefikia watu zaidi ya 1,000.
-
WHO: Ada za mazishi zinatatiza juhudi za kudhibiti Ebola Congo DR
Jul 18, 2026 09:09Umoja wa Mataifa umeonya kwamba kusafirisha miili za waathiriwa wa virusi vya Ebola kati ya maeneo mbalimbali kwa ajili ya mazishi katika miji yao kunaweza kuchangia kuenea kwa maambukizi, wakati huu ambapo idadi ya maambukizi ya virusi hivyo imeongezeka kwa takriban 70% katika wiki mbili, huku zaidi ya maambukizi 40 mapya yakirekodiwa kila siku kwa wastani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
Ebola yazidi kuwa tishio katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
Jul 17, 2026 02:57Mlipuko wa maradhi ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo unasambaa zaidi ya juhudi zinazochukuliwa za kuudhibiti huku zaidi ya watu 2,000 wakiambukizwa na zaidi ya 750 wakiwa wameaga dunia.
-
Maambukizi ya Ebola yapanda hadi zaidi ya 1,800 nchini DRC huku virusi vikisambaa hadi mkoa wa nne
Jul 11, 2026 11:28Idadi ya visa vilivyothibitishwa vya Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imevuka 1,800, kwa mujibu wa takwimu rasmi zilizotolewa siku ya Jumamosi, huku virusi hivyo vikisambaa hadi mkoa wa nne katika eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
Idadi ya vifo kutokana na maradhi ya Ebola DRC vyafikia 506
Jul 07, 2026 03:21Idadi ya vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeongezeka na kufikia 506.
-
Kenya yaisitisha ujenzi wa kituo cha Ebola cha Marekani
Jun 24, 2026 10:51Wizara ya Afya ya Kenya imesitisha ujenzi wa kituo cha karantini cha ugonjwa wa Ebola kinachozua utata, ambacho kinamilikiwa na Marekani, baada ya changamoto ya kisheria kuhoji uhalali wa mradi huo na hatari zake kwa jamii.