-
WHO: Vituo vya Ebola Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vimezidiwa
Sep 10, 2026 02:47Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, vituo vya Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vimeelemewa kutokana na kuongezeka idadi ya maambukizi ya ugonjwa huuo.
-
Watu 5 waliopona Ebola waruhusiwa kurejea nyumbani Kongo huku idadi ya maambukizi ikipindukia 6,000
Sep 01, 2026 14:15Watu watano waliopona ugonjwa wa Ebola jana waliruhusiwa kutoka katika kituo cha matibabu huko Béni, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
WHO: Mapigano yasitishwe DRC kwa angalau miezi sita ili kukomesha mripuko wa ebola
Aug 26, 2026 11:10Wakati mripuko wa ugonjwa wa ebola unaendelea kuenea kwa kasi ambayo haijawahi kushuhudiwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa wito wa kusitishwa mapigano kwa sababu za kibinadamu kwa muda wa angalau miezi sita, ili kuwezesha timu za afya kuwafikia watu walio katika hatari na kudhibiti kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa huo hatari.
-
UN yaonya: Mlipuko wa Ebola nchini DR Congo 'unaongezeka kwa kasi' baada ya zaidi ya watu 2,500 kuaga dunia
Aug 22, 2026 03:29Umoja wa Mataifa ulitangaza jana Ijumaa kwamba virusi vya Ebola vinaenea kwa kasi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kuua zaidi ya watu 2,500, ukitoa wito wa kutolewa misaada zaidi na kuonya kwamba ufadhili uliotolewa hadi sasa utaisha ndani ya wiki chache.
-
Matumaini baada ya DRC kupokea dozi 70,000 za chanjo ya Ebola
Aug 21, 2026 10:22Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, na Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa, Africa CDC, zimekaribisha uamuzi wa kuipatia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, dozi 70,000 za chanjo ya Ervebo ili kuimarisha mapambano dhidi ya mlipuko wa Ebola aina ya Bundibugyo.
-
WHO: Inawezekana kuitokomeza Ebola ndani ya miezi 3
Aug 19, 2026 09:12Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema kuwa bado kuna uwezekano wa kudhibiti mlipuko wa Ebola ambao unaenea kwa kasi inayopiku juhudi za kuuzuia, na ambao umekuwa mlipuko wa pili kwa ukubwa kuwahi kurekodiwa.
-
Mlipuko wa Ebola DRC sasa ni mbaya zaidi katika historia ya nchi hiyo
Aug 18, 2026 03:16Mlipuko wa sasa wa ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo umesababisha vifo vya watu 2,325 tangu mwezi Mei.
-
UN: Ebola inaua mtu mmoja kila baada ya nusu saa huko Congo DR
Aug 16, 2026 03:17Tom Fletcher, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Masuala ya Kibinadamu, ametangaza kwamba mlipuko wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo sasa unaua mtu mmoja kila baada ya nusu saa, akitoa wito kwa jamii ya kimataifa kuchukua hatua za haraka kupambana na mlipuko huo.
-
Mlipuko wa Ebola Kongo wapindukia maambukizi 4,000
Aug 08, 2026 02:42Idadi ya kesi za Ebola zilizothibitishwa hadi kufikia jana Ijumaa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zilikuwa zimepindukia 4,000 huku maeneo ya afya yaliyoathirika yakiongezeka.
-
Kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya Ebola DRC huku maambukizi yakienea
Aug 06, 2026 03:49Kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kimefunguliwa wiki hii na wadau wa Umoja wa Mataifa ikiwa ni hatua inayolenga kuimarisha mwitikio dhidi ya mlipuko wa sasa wa virusi vya Ebola aina ya Bundibugyo unaoendelea kuenea kwa kasi katika jimbo la Ituri, mashariki mwa taifa hilo.