Watu zaidi ya 200,000 wamepata chanjo ya ugonjwa hatari wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia (DRC) ya Kongo katika mwezi huu wa Agosti.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa serikali ya Burundi imeanza kutoa chanjo ya virusi vya ugonjwa hatari wa Ebola kwa wahudumu wa afya hususan wale wanaofanyakazi karibu na mpaka wa nchi hiyo na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC zimeunganisha nguvu kuisaidia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kupambana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Dunaini (WHO) limetangaza kuwa kwa wastani watu 86 wanaambukizwa ugonjwa wa Ebola kila wiki nchini Jamhuri ya Kdemokrasia ya Congo, DRC katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Ituri.
Serikali za Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimeazimia kushirikiana katika kukabiliana na ugonjwa hatari wa Ebola.
Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza kuwa, kumegunduliwa kesi mpya 12 za maambukizi ya maradhi ya Ebola katika mji wa Goma.
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeanzisha juhudi kubwa za kudhibiti ugonjwa hatari wa virusi vya Ebola huko mashariki mwa nchi hiyo baada ya mchimba migodi mmoja aliyekuwa na familia kubwa kuaga dunia kutokana na homa ya ugonjwa huo katika mji wa Goma.
Wasiwasi wa mlipuko mpya wa maradhi ya Ebola umetanda katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo baada ya kuripotiwa visa vitatu vipya vya maambukizi ya maradhi hayo.
Serikali ya Rwanda imefunga mpaka wake na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo baada ya kugunduliwa kesi ya tatu ya muathirika wa virusi vya ugonjwa wa Ebola katika mji wa mpakani wa Goma.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuwa ni ''dharura ya kiafya inayohitaji jumuia ya kimataifa kuitazama''.