-
Rais Yahya Jammeh atangaza hali ya hatari Gambia
Jan 18, 2017 04:11Rais Yahya Jammeh wa Gambia ametangaza hali ya hatari nchini humo kwa siku 90 akiashiria kuingiliwa na nchi ajinabi uchaguzi wa rais wa nchi hiyo uliofanyika mwezi Disemba mwaka jana.
-
Barrow ataka sherehe za kuapishwa kwake zifanyike kama ilivyopangwa, Gambia
Jan 18, 2017 04:10Rais mteule wa Gambia amesema kuwa, sherehe za kuapishwa kwake kama rais mpya wa nchi hiyo zinapaswa kufanyika kama ilivyopangwa.
-
Nchi za Afrika Magharibi kumuondoa Jammeh madarakani kwa nguvu, Gambia
Jan 17, 2017 15:10Nigeria na nchi kadhaa za Afrika Magharibi zinapanga kutuma majeshi nchini Gambia kumuondoa madarakani Rais Yahya Jammeh iwapo hatakabidhi madaraka kama ilivyopangwa.
-
Mtoto wa Rais mteule wa Gambia afariki kwa kushambuliwa na mbwa
Jan 17, 2017 07:27Mtoto wa kiume wa Rais-mteule wa Gambia mwenye umri wa miaka minane amefariki dunia kwa kushambuliwa na mbwa katika mazingira ya kutatanisha, wakati huu ambapo baba yake yuko nchini Senegal.
-
Mali yamtaka Jammeh akabidhi madaraka kwa amani
Jan 15, 2017 07:17Rais Ibrahim Boubacar Keïta wa Mali amemtaka Rais Yahya Jammeh wa Gambia akabidhi madaraka kwa amani na azuie nchi yake kutumbukia kwenye machafuko.
-
Umoja wa Afrika waitishia Gambia
Jan 14, 2017 13:21Mgogoro wa kisiasa nchini Gambia umekuwa tata zaidi katika kukaribia tarehe ya kuapichwa rais mpya wa nchi hiyo. Kuhusiana na suala hilo Umoja wa Afrika (AU) umemtishia Rais wa Gambia kuwa hautamtambua rasmi kuwa rais halali tangu tarehe iliyoanishwa kwa ajili ya kufanyika sherehe za kumuapisha rais mteule wa nchi hiyo.
-
UNOWAS kuhakikisha Jammeh anaondoka madarakani nchini Gambia
Jan 14, 2017 07:29Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa Afrika Magharibi amesema kunafanyika jitihada za kumshawishi Yahya Jammeh aliyeshindwa katika uchaguzi wa rais Gambia kuondoka madarakani na kumuachia mshindi, Adama Barrow, achukue hatamu za uongozi nchini humo.
-
Adama Barrow asema yuko tayari kufanya mazungumzo na Jammeh
Jan 13, 2017 08:07Mshindi wa uchaguzi wa Rais nchini Gambia, Adama Barrow amesema yuko tayari kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na Rais Yahya Jammeh, ambaye alipinga matokeo hayo.
-
Bunge la Wawakilishi Nigeria lafungua njia ya kumpa hifadhi ya kisiasa Rais wa Gambia
Jan 12, 2017 16:54Bunge la Wawakilishi la Nigeria leo limepiga kura kuidhinisha uamuzi wa kumpatia hifadhi ya kisiasa Rais Yahya Jammeh wa Gambia endapo atakubali kung'atuka madarakani.
-
Mahakama Kuu ya Gambia yakataa kusikiliza shauri la malalamiko ya uchaguzi
Jan 11, 2017 04:06Mahakama Kuu ya Gambia imetangaza kuwa katika hali ya sasa haiwezi kusikiliza na kutoa uamuzi kuhusu malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais wa nchi hiyo.