-
"Mateka wa vita wa Iran ni nembo ya Muqawama dhidi ya adui"
Aug 16, 2024 07:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, Mafungwa wa Vita ni nembo ya Muqawama na kusimama kidete taifa kubwa la Jamhuri ya Kiislamu dhidi ya ubeberu na utwishaji wa maadui wa taifa hili.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu alihimiza taifa la Iran kusimama kidete katika vita vya kisaikolojia vya adui
Aug 15, 2024 06:35Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei, amezungumzia hila na njama za wasiolitakia mema taifa la Iran katika kuanzisha vita vya kisaikolojia na kutaka kulirudisha nyuma katika nyuga mbalimbali na kusema, utambuzi wa uwezo wa ndani na kuepuka kutia chumvi nguvu za maadui ndiyo njia pekee ya kukabiliana na njama hizo.
-
Jenerali Ghorbani: Vikwazo vimeimarisha mfumo wa kijeshi wa Iran
Aug 15, 2024 04:15Naibu Mratibu wa Kikosi cha Nchi Kavu cha Jeshi la Iran amesema kuwa vikwazo vya kikatili dhidi ya Iran havijakuwa na matokeo mengine ghairi ya kuimarisha mifumo ya kijeshi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Bin Salman ahofia kuuawa kwa kufuatilia mpango wa kuanzishwa uhusiano rasmi kati ya Saudia na Israel
Aug 15, 2024 00:15Mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman ameripotiwa kuwa anahofia "kuuawa" kwa sababu ya juhudi zake za kutaka kuhakikisha ufalme huo unaanzisha uhusiano rasmi na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Muqawama Iraq: Jibu la Iran dhidi ya Israel litakuwa la nguvu
Aug 14, 2024 23:16Mkuu wa Baraza la Kisiasa la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya al-Nujabaa ya Iraq amesema jibu tarajiwa la Iran kwa mauaji ya kigaidi yaliyofanywa mwezi uliopita na utawala wa Kizayuni dhidi ya Ismail Haniyah, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS litakuwa la nguvu, lenye taathira na la kimahesabu.
-
Iran yatuma barua za malalamiko kwa maafisa wa haki za binadamu wa UN
Aug 14, 2024 11:27Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi amewatumia barua kwa nyakati tofauti maafisa wa haki za binadamu akibainisha malalamiko makubwa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa hatua na sera zisizo z akibinadamu za utawala wa Kizayuni na hasa mauaji ya kigaidi ya Ismail Haniyeh kiongozi wa kisiasa wa Hamas.
-
Kiongozi Muadhamu atilia mkazo wajibu wa kusimama imara mbele ya vita vya kisaikolojia vya adui
Aug 14, 2024 09:00Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametilia mkazo wajibu wa kusimama imara kukabiliana na vita vya kisaikolojia vya adui akisema kuwa, wanaoendesha vita hivyo dhidi ya Iran wanajaribu kuzusha hofu na kulifanya taifa hili lilegeze kamba na lirudi nyuma katika nyuga tofauti.
-
Bagheri Kani: Uvamizi wa Wazayuni katika Msikiti wa Al-Aqsa unalenga kuzidisha mivutano
Aug 14, 2024 04:07Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uvamizi wa baadhi ya mawaziri wa serikali ya utawala bandia wa Israel na walowezi wa Kizayuni katika msikiti wa al Aqsa ni hatua ya kichochezi inayolenga kushadidisha mivutano na ukosefu wa amani katika eneo.
-
Iran: Marekani ndiye muungaji mkono na muenezaji mkuu wa ugaidi katika eneo na dunia
Aug 13, 2024 02:11Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema, Marekani ndiyo muungaji mkono na muenezaji mkuu wa ugaidi katika eneo na dunia.
-
Iran: Hatutaruhusu Israel ichochee moto wa vita Asia Magharibi
Aug 11, 2024 04:05Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inafanya hima kuzuia utawala wa Kizayuni wa Israel utimize ndoto yake ya kuwasha na kuchochea moto wa vita vya pande zote katika eneo la Asia Magharibi.