-
Iran: Marekani ilikuwa na taarifa kuhusu Operesheni ya Ahadi ya Kweli ya kuutia adabu utawala wa Israel
Apr 18, 2024 04:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Jamhuri ya Kiislamu iliikuwa imeshaitaarifu serikali ya Marekani kabla ya kutekeleza Operesheni ya Ahadi ya Kweli ya kuutia adabu utawala wa Israel mfanyamauaji ya kimbari.
-
Borrell: Ukraine isiombe kupewa msaada na Magharibi kama iliopewa Israel katika shambulio la Iran
Apr 18, 2024 02:19Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya Josep Borrell amesema, Ukraine haipaswi kuomba msaada wa aina ile ile ambayo nchi za Magharibi zilitoa kwa Israel wakati wa shambulio la kijeshi la Iran kwa sababu hali hizo mbili haziwezi kulinganishwa.
-
Iran iliwasiliana na nchi za eneo katika kutekeleza Operesheni ya Ahadi ya Kweli dhidi ya Israel
Apr 17, 2024 07:19Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema: Iran ilikuwa ikiwasiliana na nchi za eneo katika mchakato wa kutoa jibu kwa utawala wa Kizayuni na utekelezaji wa Operesheni ya Ahadi ya Kweli.
-
Grossi asisitiza tena kutokuwepo shughuli za kijeshi za nyuklia nchini Iran
Apr 16, 2024 22:58Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA amesisitiza kuwa, hakuna nyaraka zozote zinazothibitisha utengenezaji wa silaha za nyuklia nchini Iran na kuwa, mivutano ya hivi sasa haijavuruga mchakato wa ufuatiliaji wa wakala huo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.
-
Amir-Abdollahian: Iran haitoruhusu Israel kuhatarisha usalama wa ukanda huu
Apr 16, 2024 07:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaamini kwamba usalama na utulivu wa nchi za eneo hili zima ni muhimu sana kwake, bali ni sawa kabisa na usalama wake yenyewe na haitoruhusu utawala wa Kizayuni kuhatarisha usalama wa eneo hili kwa chokochoko zake.
-
Kikao cha Baraza la Usalama: Uwanja wa makabiliano kati ya waungaji mkono wa Iran na Wamagharibi wanaounga mkono utawala wa Kizayuni.
Apr 16, 2024 04:24Kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kujadili mashambulizi ya Iran ya kuuadhibu utawala wa Israel kilifanyika Jumapili jioni tarehe 14 Aprili, kikao ambacho kilibadilika na kuwa uwanja wa makabiliano kati ya nchi zinazounga mkono Iran na kambi ya Magharibi waitifaki wa utawala wa Kizayuni.
-
Onyo la Iran kwa Marekani na Magharibi kuhusu madhara yatakayozipata zikiiunga mkono Israel
Apr 15, 2024 08:32Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeionya na kuitahadharisha Marekani na nchi za Magharibi juu ya kuuunga mkono kijeshi utawala wa Kizayuni na kufanya chokochoko dhidi ya Iran na kutangaza kwamba, iwapo nchi hizo zitaingilia kati katika kuuunga mkono utawala wa Kizayuni, vituo vyao vyote na maeneo yote ya maslahi yao yatashambuliwa na vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Iran haitasita kulinda maslahi yake
Apr 15, 2024 01:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitasita wala kuwa na shaka katika kulinda maslahi yake halali dhidi ya uchokozi wowote mpya.
-
Rais Raisi: Hatua yoyote ya kifidhuli itakabiliwa na jibu kali zaidi la Iran
Apr 14, 2024 07:42Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utafanya harakati yoyote ya kifidhuli utakabiliwa na jibu madhubuti, zito na kali zaidi.
-
Balozi wa Iran UN: Jibu la Iran litakuwa kali zaidi iwapo Israel itaanzisha tena mashambulizi
Apr 14, 2024 04:15Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ametangaza katika barua kwa Baraza la Usalama kwamba ikiwa utawala wa Israel utaanzisha tena mashambulizi yoyote ya kijeshi, bila shaka jibu la Iran litakuwa la nguvu na kali zaidi.