-
Khalid Mash'al: Karibuni hivi, vita vya miezi sita vitamvunja adui Mzayuni
Apr 13, 2024 23:01Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya ughaibuni ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS Khaled Mash'al, amepongeza istiqama ya kishujaa ya Ukanda wa Ghaza na kusisitiza kuwa vita vya miezi sita wanavyopigana Wapalestina na utawala wa Kizayuni wa Israel "karibuni hivi vitamvunja adui Mzayuni".
-
Ombi la Rais wa Marekani kwa Iran: Msiishambulie Israel
Apr 13, 2024 08:39Rais wa Marekani kwa mara nyingine tena, katika uingiliaji wa wazi na kuunga mkono utawala wa Israel, ameiomba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran isijibu mashambulizi ya utawala huo kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus huko Syria.
-
Raisi: Madola ya kibeberu yanazusha fitna ili kuvuruga usalama kati ya Iran na Pakistan
Apr 12, 2024 07:48Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, kustawishwa uhusiano wa Iran na Pakistan hakufurahishi madola ya kibeberu na kwa hivyo yanazusha fitna ili kuleta mpasuko kati ya mataifa hayo mawili na nchi hizo mbili za Kiislamu.
-
Mwakilishi wa Iran UN asisitiza ulazima wa kuuadhibu utawala vamizi wa Israel
Apr 12, 2024 04:10Ofisi ya Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa imesema Baraza la Usalama lilipaswa kulaani mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya maeneo ya kidiplomasia ya Iran huko Damascus, mji mkuu wa Syria.
-
Amir Abdollahian: Kujilinda kwa lengo la kumuadhibu mchokozi ni jambo la lazima
Apr 11, 2024 23:57Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Jamhuri ya Kislamu ya Iran amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel unapokiuka kikamilifu kinga ya watu binafsi na maeneo ya kidiplomasia kwa kukanyaga sheria za kimataifa na Mikataba ya Vienna, inakuwa lazima kujihami kwa lengo la kumuadhibu mchokozi.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Imarati, Uturuki wajadiliana matukio ya Ghaza
Apr 11, 2024 06:24Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika mazungumzo yake ya simu na mawaziri wenzake wa Muungano wa Falme za Kiarabu (Imarati) na Uturuki kwamba kuna udharura wa kukomeshwa haraka jinai za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.
-
Rais Raisi: Kukata uhusiano wa kiuchumi na kisiasa ndiyo silaha bora ya kuipigisha magoti Israel
Apr 10, 2024 23:09Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kukatwa uhusiano wa kiuchumi na kisiasa wa nchi za Waislamu na utawala wa Kizayuni ndiyo silaha bora ya kukomesha jinai za Wazayuni huko Palestina.
-
Kiongozi Muadhamu: Ghaza ndiyo kadhia kuu ya Ulimwengu wa Kiislamu hivi sasa
Apr 10, 2024 10:45Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, Ghaza ni suala ambalo haliwezi kufumbiwa macho kwani ndiyo kadhia kuu ya Ulimwengu wa Kiislamu hivi sasa, hivyo kila mmoja wetu anapaswa kutekeleza vizuri majukumu yake kuhusu Ukanda wa Ghaza.
-
Kiongozi Muadhamu: Israel ilifanya makosa, 'itaadhibiwa' kwa kushambulia ubalozi mdogo wa Iran
Apr 10, 2024 04:22Kiongozi Muadhamu wa wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei anasema utawala wa Kizayuni wa Israel "lazima uadhibiwe na kutiwa adabu" kwa shambulio lake baya dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran katika mji mkuu wa Syria, Damascus.
-
Abdollahian: Marekani inapasa kuwajibishwa kwa shambulio dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran
Apr 09, 2024 04:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameeleza kuwa serikali ya Marekani ina jukumu na inapasa kubeba dhima kwa shambulio la kigaidi katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus lililofanywa na utawala wa Israel unaotekeleza mauaji ya kimbari huko Gaza.