Jan 23, 2021 11:49
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemuasa Rais mpya wa Marekani Joe Biden, ahitimishe sera za mashinikizo zilizogonga mwamba za mtangulizi wake Donald Trump na kusisitiza kuwa, "dirisha la fursa kwa timu mpya ya Ikulu ya White House halitabakia wazi milele."