Jan 08, 2020 02:51
Muungano eti wa kupambana na kundi la Daesh unaoongozwa na Marekani umehamisha makao yake makuu kutoka Iraq na kuyapeleka Kuwait kufuatia mauaji ya Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Luteni Jenerali Qassem Soleimani na Naibu Kamanda wa kikosi cha kujitolea cha wananchi wa Iraq, al Hashdul Shaabi Abu Mahdi al Muhandes, na sisitizo la Iran la kulipiza kisasi mauaji hayo ya kigaidi yaliyofanywa na Marekani.