Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitizia ulazima wa kufanyika uchunguzi wa kimataifa kuhusiana na uharibifu, utesaji na mauaji yaliyofanywa na jeshi la Kizayuni katika Hospitali ya Al-Shifa huko Ukanda wa Ghaza.
Mkutano wa pande tatu wa mawaziri wa mambo ya nje wa Misri, Jordan na Ufaransa ulifanyika Jumamosi Cairo, mji mkuu wa Misri, kuhusiana na matukio ya hivi karibuni katika vita vya Gaza na mashauriano ya kusitisha mapigano hayo.
Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani [CAIR] limetoa wito kwa Umoja wa Mataifa kuchunguza video inayoonyesha wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wakiwapiga risasi bila sababuu Wapalestina wawili wanaoonekana kuwa hawana silaha kisha kuzifukia maiti zao kwa buldoza.
Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) zimekosoa uungaji mkono na himaya kubwa ya Marekani kwa utawala wa Kizayuni wa Israel na kimya cha viongozi wa nchi za Kiislamu kuhusiana na jinai zinazofanywa na utawala huo ghasibu.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini amesema kuwa kutotekelezwa maamuzi ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki dhidi ya Israel kunaidhoofisha mahakama hiyo.
Mshauri wa zamani wa Ikulu ya Marekani (White House) Jared Kushner amesema, utawala wa Kizayuni wa Israel inapasa uwaondoe Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza na kuwahamishia kwenye jangwa la Negev kusini mwa ardhi zilizopachikwa jina bandia la Israel.
Msemaji wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ameitahadharisha Israel kuhusu oparesheni yoyote ya kijeshi katika mji wa Rafah na kusema, misaada ambayo imewasili Ukanda wa Gaza haitoshi kukidhi mahitaji ya wakazi wa eneo hilo.
Kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni katika kivuli cha uungaji mkono wa Marekani kwa utawala huo na kufungwa njia za kufikisha misaada na kuingia chakula na dawa katika Ukanda wa Gaza kumesababisha kuongezeka la idadi ya mashahidi wa Palestina.
Kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza kumepelekea kuongezeka idadi ya Wapalestina wanaouawa shahidi na miundombinu inayobomolewa na kuteketezwa katika eneo hilo.
Miezi 5 ya vita dhidi ya Ukanda wa Gaza ambavyo vilikuwa havijawahi kushuhudiwa tena imekuwa na matokeo mbalimbali katika ngazi ya ndani, kikanda na kimataifa.