-
Maandamano ya vijana yamlazimisha Ruto kuweka kando Muswada wa Fedha 2024
Jun 26, 2024 15:05Rais William Ruto wa Kenya amesema kwamba hatatia saini Muswada wa Fedha 2024 kuwa sheria. Ni baada ya maandamano makubwa ya siku kadhaa yaliyofuatiwa na mauaji ya waandamanaji mjini Nairobi jumanne ya jana.
-
Watu 10 wameuawa Nairobi wakati polisi ilipowafyatulia risasi waandamanaji waliovamia bunge
Jun 26, 2024 02:51Watu 10 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa jana Jumanne wakati polisi walipowafyatulia risasi mamia ya waandamanaji waliovamia majengo ya bunge jijini Nairobi, mji mkuu wa Kenya, kupinga sheria ya iliyopitishwa na wabunge ya kuongeza ushuru.
-
Mamia ya askari polisi wa Kenya watumwa Haiti licha ya ukosoaji
Jun 25, 2024 10:42Askari polisi 400 wa Kenya wameelekea nchini Haiti leo Jumanne kwa ajili ya kwenda kulinda usalama na kurejesha uthabiti katika nchi hiyo ya Caribbean.
-
Kenya yaruhusu kufanyika maandamano kwa masharti
Jun 25, 2024 07:44Kithure Kindiki Waziri wa Usalama wa Ndani wa Kenya amewataka vijana wanaoandamana kupinga Muswada wa Fedha wa 2024 kuimarisha amani na usalama, kutobeba aina yoyote ya silaha kutakiwa kuondoka katika maeneo ya mikusanyiko ifikapo saa kumi na mbili jioni.
-
Mudavadi: Kuweka kando Muswada wa Fedha ni sawa na kuangusha Serikali ya Kenya
Jun 22, 2024 06:49Kinara wa Mawaziri wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema Muswada wa Fedha 2024 lazima upitishwe na kutiwa saini na Rais William Ruto kuwa sheria, akisema kinyume na hivyo itakuwa ni sawa na kuangusha Serikali.
-
Polisi wa Kenya washutumiwa kwa kumuua mmoja wa waandamanaji Nairobi
Jun 21, 2024 07:57Asasi za kiraia na mashirika ya kutetea haki za binadamu yameijia juu polisi ya Kenya kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga risasi mmoja wa waandamanaji wanaopinga mpango wa kuongeza ushuru, kodi na tozo.
-
Marekani kuipa Kenya hadhi ya mshirika wake mkuu asiye mwanachama wa NATO
May 23, 2024 07:20Rais Joe Biden wa Marekani anatarajiwa kuipa Kenya hadhi ya mshirika wake mkuu asiye mwanachama wa NATO wakati wa ziara ya kiserikali ya siku tatu ya Rais wa Kenya William Ruto nchini humo, ambaye amekaribishwa na Biden katika Ikulu ya White House mapema leo kabla ya mapokezi rasmi yatakayoanza kwa ukaguzi wa gwaride la heshima na kufikia kielele chake kwa dhifa ya kifahari ya chakula cha usiku.
-
Polisi 200 wa Kenya kupelekwa Haiti Alkhamisi ijayo
May 18, 2024 04:00Polisi 200 wa Kenya watapelekwa nchini Haiti kulinda usalama siku ya Alkhamisi ijayo. Ni baada ya vuta nikuvute ya muda mrefu mahakamani, ambapo Januarii mwaka huu Mahakama ya juu nchini Kenya ilitangazwa kuwa, mpango wa serikali wa kutuma polisi nchini Haiti kuongoza kikosi cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa ni kinyume na katiba.
-
Kenya na Uganda zaafikiana kuhusu ujenzi wa bomba la mafuta
May 17, 2024 07:24Kenya na Uganda zimekubaliana kujenga kwa pamoja bomba la kusafirishia mafuta kutoka mjini Eldoret katika eneo la Bonde la Ufa nchini Kenya hadi Uganda.
-
Ripoti yafichua: Chama tawala Kenya kiliazimia kuua Azimio la Umoja-One Kenya
May 10, 2024 09:54Vyombo vya habari vya Kenya vimefichua kuwa, mabadiliko ya siri yaliyotayarishiwa miswada ya kufanikisha utekelezaji wa ripoti ya Kamati ya Kitaifa ya Mazungumzo (NADCO) iliyowasilishwa majuzi katika Seneti ya nchi hiyo yamefuchua njama ya kuvunja chama cha Azimio la Umoja-One Kenya kinachoongozwa na Raila Odinga.