-
Iran yaonya baada ya Israel kutishia kushambulia ndege yake ya abiria
Feb 15, 2025 03:45Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei ameukosoa vikali utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kutishia kushambulia ndege ya abiria ya Iran iliyokuwa imebeba raia wa Lebanon.
-
Bunge la Libya lalaani njama za Wazayuni za kuwahamisha watu wa Ghaza
Feb 09, 2025 07:07Bunge la Libya limelaani na kupinga njama za Marekani na Israel za kutaka kuwahamisha wananchi wa Ghaza na kuwapeleka sehemu nyingine nje ya ardhi zao za jadi za Palestina.
-
Lebanon yaunda serikali ya kwanza baada ya zaidi ya miaka miwili
Feb 09, 2025 03:39Lebanon imeunda serikali yake ya kwanza kamili tangu mwaka 2022, wakati huu ambapo nchi hiyo ya Kiarabu inajitahidi kujenga upya eneo lake la kusini lililoharibiwa na vita; na kuhakikisha usalama unarejea baada ya mapigano kati ya Israel na Harakati ya Muqawama ya Hizbullah.
-
Joseph Aoun: Kuondoka jeshi la Israel ni ufunguo wa kurejea amani Lebanon
Feb 08, 2025 04:33Rais wa Lebanon amesisitiza katika mazungumzo na Mjumbe wa Marekani kuwa amani itarejea kusini mwa Lebanon iwapo jeshi la utawala wa Kizayuni litaondoka katika eneo hilo.
-
Israel yashambulia Lebanon, yakiuka makubaliano ya usitishaji vita
Feb 07, 2025 04:22Jeshi la Israel limefanya mashambulizi kadhaa ya anga dhidi ya maeneo tofauti ya kusini na mashariki mwa Lebanon, huo ukiwa ni ukiukaji mkubwa na wa wazi wa makubaliano ya kusitisha mapigano kati yake na nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Kiongozi Muadhamu amteua Naim Qassem kuwa mwakilishi wake Lebanon
Feb 05, 2025 08:59Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, katika dikrii, amemuarifisha Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawamaya ya Hizbullah, Sheikh Naim Qassem kama mwakilishi wake nchini Lebanon.
-
Mkuu wa Hizbullah: Lebanon haitasahau msaada wa Iran, Iraq wakati wa vita vya Israel
Jan 28, 2025 04:33Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, watu wa Lebanon hawatasahau uungaji mkono na msaada mkubwa waliopewa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Iraq wakati wa mashambulizi makali ya anga na nchi kavu ya Israel dhidi ya nchi yao.
-
Imam Khamenei apongeza ujasiri wa wananchi wa Lebanon
Jan 27, 2025 09:51Akaunti rasmi ya mtandao wa kijamii wa X ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei imetuma ujumbe kufuatia kitendo cha kijasiri cha wananchi wa Lebanon kusini mwa nchi hiyo ya Kiarabu.
-
UNIFIL yasisitiza kuondoka Lebanon wanajeshi wa Israel
Jan 27, 2025 03:38Kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa kusini mwa Lebanon (UNIFIL) kimetaka kuondoka kikamilifu wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel huko kusini mwa Lebanon.
-
"Hatutajadili mamlaka ya Lebanon", asema Rais Aoun baada ya Israel kuua Walebanon 15
Jan 26, 2025 22:55Rais wa Lebanon, Joseph Aoun amesema "mamalaka ya kujitawala Lebanon na ardhi yake ni jambo lisiloweza kujadiliwa". Amesema hayo baada ya vikosi vya Israel kuwafyatulia risasi na kuwaua Walebanon waliokuwa wamekimbia makazi yao kusini mwa Lebanon na waliokuwa wakirejea katika miji yao, huku muhula wa mwisho wa kuondoka askari hao makatili ukimalizikka.