-
"Hatutajadili mamlaka ya Lebanon", asema Rais Aoun baada ya Israel kuua Walebanon 15
Jan 26, 2025 22:55Rais wa Lebanon, Joseph Aoun amesema "mamalaka ya kujitawala Lebanon na ardhi yake ni jambo lisiloweza kujadiliwa". Amesema hayo baada ya vikosi vya Israel kuwafyatulia risasi na kuwaua Walebanon waliokuwa wamekimbia makazi yao kusini mwa Lebanon na waliokuwa wakirejea katika miji yao, huku muhula wa mwisho wa kuondoka askari hao makatili ukimalizikka.
-
Iran yakanusha tuhuma za Israel za kupeleka silaha Lebanon
Jan 25, 2025 08:05Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amepuuzilia mbali madai ya Israel kamba Jamhuri ya Kiislamu inasafirisha kimagendo silaha kwenda Lebanon.
-
Israel haitaondoa askari wake kusini mwa Lebanon kama ilivyoafikiwa, Marekani yaiunga mkono
Jan 25, 2025 02:44Vyombo vya habari vya Kiebrania vimeripoti kuwa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel halitaondoka kusini mwa Lebanon utakapomalizika muhula uliowekwa wa siku 60 kesho Jumapili kulingana na makubaliano ya kusitisha vita yaliyofikiwa kati ya Israel na harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Lebanon ya Hizbullah.
-
Gazeti la Kiebrania la Haaretz: Israel imeidhinisha mpango wa kuondoa askari wake Ukanda wa Ghaza
Jan 12, 2025 23:56Gazeti la Kiebrania la Haaretz limeripoti kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel umeidhinisha mipango ya kuwaondoa wanajeshi katika Ukanda wa Ghaza, baada ya hatua zilizopigwa katika mazungumzo ya kubadilishana mateka na harakati ya Hamas.
-
Pezeshkian ampongeza Rais mpya wa Lebanon; asisitiza umoja na kuimarisha utulivu
Jan 10, 2025 23:28Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemtumia ujumbe Rais mpya wa Lebanon na kusisitiza kuwa umoja na kuimarisha utulivu vitazima njama za kujitanua na tamaa za adui Mzayuni dhidi ya Lebanon.
-
Iran yapongeza kuchaguliwa rais mpya nchini Lebanon, yasisitiza kustawishwa uhusiano
Jan 10, 2025 07:00Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amempongeza Rais mpya wa Lebanon, Serikali na wananchi wake pamoja na mirengo na vyama vyote husika katika uga wa kisiasa wa nchi hiyo kwa kuchaguliwa rais mpya.
-
Waziri Mkuu wa Lebanon: Lazima Israel iondoke kikamilifu kusini mwa Lebanon kabla ya Januari 26
Jan 08, 2025 00:00Waziri Mkuu wa Lebanon Najib Miqati amesema Beirut imefikisha "salamu za wazi kabisa" kwa waangalizi wa kimataifa wa makubaliano ya kusitisha mapigano na Israel kwamba utawala huo wa Kizayuni lazima uondoe kikamilifu vikosi vyake kusini mwa Lebanon kabla ya mwisho wa Januari.
-
Droni za Yemen zahepa mifumo ya utunguaji ya utawala wa Kizayuni, zapiga Tel Aviv na Ashkelon
Dec 14, 2024 02:57Vikosi vya Jeshi la Yemen vimetangaza kuwa vimefanya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani kulenga mji wa Jaffa karibu na Tel Aviv pamoja na mji wa Ashkelon katika eneo la kati la ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu katika operesheni mpya dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Waziri wa Lebanon: Israel imefanya uhalifu wa kivita wa kimazingira
Dec 13, 2024 22:58Waziri wa Mazingira wa Lebanon amesema kuwa Israel imeharibu ardhi na misitu ya kusini mwa hiyo kwa kutumia silaha zilizopigwa marufuku.
-
Sheikh Naim Qassim: Muqawama uko imara na umepata ushindi
Dec 06, 2024 00:21Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, muqawama ukitegemea nguvu na uwezo wa wapiganaji wake umepata ushindi katika vita dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.