-
Waziri wa Sheria wa Libya anusurika kuuawa katika shambulio la watu wenye silaha
Jan 29, 2022 04:46Vyombo vya habari vimetangaza kuwa Waziri wa Sheria wa Libya amenusurika kuuawa katika shambulio la watu wenye silaha lililotokea kwenye barabara ya As-Sawani katika mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli.
-
Mjumbe Maalumu wa UN Libya: Kipaumbele kikuu ni maridhiano ya kitaifa
Jan 16, 2022 23:08Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya amesema kuwa, kipaumbeke kikuu zaidi hivi sasa kuhusu Libya ni kuweko maridhiano ya kitaifa na kusisitiza kuwa wananchi wa Libya hawataki tena vita.
-
Jenerali Haftar, mbabe wa kivita wa Libya aitembelea Israel
Jan 16, 2022 04:24Mbabe wa kivita na jenerali muasi wa Libya Khalifa Haftar ameripotiwa kufanya safari ya siri ya kuutembelea utawala wa Kizayuni wa Israel, huku duru za habari zikieleza kuwa maafisa wa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika wanaandamwa na mashinikizo ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala huo bandia.
-
Waziri Mkuu wa Libya akanusha madai ya kukutana na maafisa wa Israel
Jan 13, 2022 23:35Kaimu Waziri Mkuu wa serikali ya mpito ya umoja wa kitaifa ya Libya amekadhibisha madai kuwa amekutana na kufanya mazungumzo na maafisa wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Algeria yaufungua tena ubalozi mdogo nchini Libya
Jan 11, 2022 10:33Algeria imefungua tena ubalozi wake mdogo huko Tripoli mji mkuu wa Libya baada ya kufungwa kwa miaka minane.
-
Tarehe mpya ya Uchaguzi wa Rais nchini Libya
Jan 05, 2022 06:31Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Libya imetangaza tarehe 24 mwezi huu wa Januari 2022 kuwa siku ya kufanyika uchaguzi wa rais nchini humo licha ya kwamba bado kuna hitilafu kuhusu wakati hasa unaopaswa kufanyika uchaguzi huo.
-
Tume ya uchaguzi Libya: Uchaguzi mkuu utafanyika tarehe 24 Januari
Jan 03, 2022 23:18Tume Kuu ya Taifa ya Uchaguzi nchini Libya (HNEC) imetangaza kuwa uchaguzi mkuu wa nchi hiyo uliokuwa umeakhirishwa, utafanyika tarehe 24 ya mwezi huu wa Januari.
-
Bunge la Libya lapendekeza uchaguzi wa rais uakhirishwe kwa miezi sita
Dec 29, 2021 00:53Baraza la Wawakilishi (Bunge) la Libya limependekeza kuwa ucahguzi wa rais nchini humo uakhirishwe kwa miezi sita.
-
Libya yamtaja balozi wa Uingereza kuwa hatakikani nchini humo
Dec 28, 2021 04:04Bunge la Libya limemtaja balozi wa Uingereza nchini humo kuwa ni mtu asiyetakikana nchini humo. Hatua hiyo imechukuliwa baada ya matamshi yaliyotolewa na balozi wa Uingereza yaliyotambuliwa kuwa yamekiuka sheria za kimataifa.
-
Baada ya kuahirishwa uchaguzi wa rais, Libya yaunda kamati ya Bunge ya kubuni ramani mpya ya njia
Dec 24, 2021 12:23Baraza la Wawakilishi la Libya limeunda kamati ya wajumbe 10 ili kubuni ramani mpya ya njia baada ya kuahirishwa uchaguzi uliokuwa umepangwa kufanyika leo, Ijumaa.