-
Iran haifanyi mazungumzo yoyote na utawala wa Marekani
Jun 08, 2018 09:48Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema maadamu Marekani haitumii lugha ya heshima na haiachi kutumia vitisho wakati wa kuzungumza na taifa kongwe na lenye ustaarabu la Iran, basi hakuna uwezekano wowote wa kuwepo mazungumzo katika uga wowote baina ya Iran na Marekani.
-
Utafiti: US imeshadidisha matumizi ya drone katika utawala wa Trump
Jun 08, 2018 02:46Utafiti mpya unaonesha kuwa, matumizi ya ndege zisizo na rubani (drone) za Marekani zenye silaha hatari yameongezeka katika utawala wa Donald Trump.
-
Zarif: Nchi wanachama wa JCPOA zifidie hasara ilizopata Iran bila kutoa masharti yoyote
Jun 08, 2018 00:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: Ili makubaliano ya nyuklia ya JCPOA yaendelee, lazima nchi zilizosalia kwenye makubaliano hayo pamoja na washirika wengine wa kibiashara watoe hakikisho kwamba hasara ilizopata Iran (kutokana na Marekani kujitoa kwenye JCPOA) zinafidiwa bila masharti yoyote kupitia hatua za kitaifa, kieneo na kimataifa.
-
Putin: Hatutaruhusu Marekani ijifanye polisi wa dunia
Jun 08, 2018 00:05Rais Vladimir Putin wa Russia amesema, hatua za upande mmoja za rais wa Marekani ndio chanzo hasa cha kuongezeka mivutano duniani.
-
Hatua mpya za Ulaya kulinda makubaliano ya JCPOA
Jun 07, 2018 05:23Sambamba na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutangaza hatua ya kuimarisha shughuli zake za nyuklia katika fremu ya mapatano ya nyuklia na nchi sita kubwa za dunia mashuhuri kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA), nchi za Ulaya zimeongeza mashauriano na juhudi za kuyalinda yasije yakasambaratika.
-
Kufichuliwa njama ya Marekani ya kuingiza tena magaidi nchini Iraq
Jun 07, 2018 02:21Matukio ya mwaka mmoja uliopita nchini Iraq ambapo magaidi wakufurishaji wa ISIS au Daesh wamesambaratishwa na kutumiliwa kikamilifu kutoka maeneo yote waliyokuwa wameyateka kufuatia jitihada za jeshi na makundi ya kujitolea ya wananchi, yameiandaa Iraq kuingia duru mpya ya baada ya Daesh na kuandaa mazingira ya uchaguzi wa bunge uliofanyika mwezi uliopita.
-
Jaji wa Marekani: Yumkini Trump akauzuliwa kutokana na kesi ya ufuska
Jun 06, 2018 02:53Jaji mmoja nchini Marekani amesema huenda Rais Donald Trump akauzuliwa iwapo atapatikana na hatia katika kesi ya ufuska iliyowasilishwa na mwanamke mmoja ambaye anadai kudhalilishwa naye kingono.
-
Marekani kupanua operesheni zake za kijeshi Yemen kufuatia ombi la Imarati
Jun 04, 2018 09:48Marekani inatathmini ombi la Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) la kuipa msaada wa moja kwa moja kwa ajili ya kufanikisha mashambulizi ya kuiteka bandari ya Hudaydah, ambayo kwa sasa inadhibitiwa na vikosi vya Ansarullah vya Yemen.
-
Shamkhani: Trump ameifanya US itengwe kisiasa kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa
Jun 03, 2018 10:29Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Kushamiri vitendo vya ukatili vya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza na Ufukwe wa Magharibi wa Mto Jordan ni hatua ya kutapatapa inayochukuliwa baada ya kushindwa mpango na njama ya kuwatumia magaidi wa kitakfiri ili kuzusha mapigano katika Ulimwengu wa Kiislamu.
-
(Hatua kwa hatua kuelekea Siku ya Kimataifa ya Quds): Dhulma wanayofanyiwa Wapalestina na madai ya haki za binadamu ya Marekani
Jun 03, 2018 02:11Vitendo vilivyo dhidi ya ubinadamu ambavyo Israel inawafanyia wananchi madhulumu wa Palestina ni miongoni mwa mambo ambayo mara kwa mara yamekuwa yakifanywa ajenda za Baraza la Haki za Binadamu la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa; hata hivyo mara zote Marekani imekuwa ikiingilia kati na kuzuia kupasishwa maazimio ya kimataifa ya kulaani jinai hizo za Israel.