-
Marekani yakiri kuwa haiwezi kuingia kwenye vita vya kijeshi na Iran
Dec 17, 2017 04:26Waziri wa Ulinzi wa Marekani amekiri kuwa Washington haina mpango wowote wa kuanzisha vita vya kijeshi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutokana na tuhuma kuwa Tehran inaizatiti kwa silaha harakati ya Ansarullah ya Yemen.
-
Putini afichua ushirikiano wa Marekani na magaidi huko Syria
Dec 16, 2017 00:15Rais wa Russia amefichua kuwa wanajeshi wa Marekani walioko nchini Syria walikuwa wakiwaunga mkono na kuwapatia silaha magaidi na ndio waliokuwa wakikwamisha kusambaratishwa magaidi hao.
-
Ripoti: Marekani na Saudi Arabia zimewapa magaidi wa ISIS silaha
Dec 15, 2017 03:12Shirika moja la kimataifa limezilaumu tawala za Marekani na Saudi Arabia kuwa zimekuwa zikiwafikishia magaidi wa ISIS silaha kwa siri kupitia makundi ya wapinzania nchini Syria.
-
Jumuiya ya NAM yakosoa hatua ya Marekani dhidi ya Quds
Dec 13, 2017 11:55Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM) imekosoa vikali hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuitambua Quds kuwa eti mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Tillerson: Niko tayari kufanya mazungumzo na Korea ya Kaskazini
Dec 13, 2017 04:24Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani ametangaza kuwa Washington ina hamu ya kufanya mazungumzo na Pyong Yang bila ya sharti lolote kuhusu kuipokonya silaha Korea ya Kaskazini.
-
Marekani iko tayari Bashar Assad aendelee kubakia madarakani hadi mwaka 2021
Dec 13, 2017 00:21Ripoti za baadhi ya duru za habari nchini Marekani zinaeleza kuwa baada ya kukata tamaa ya kumwondoa madarakani Rais Bashar Al Assad wa Syria, serikali ya Washington imechukua uamuzi mpya wa kuafiki Assad aendelee kuwa rais wa Syria hadi mwaka 2021.
-
Wabunge 56 wanawake wa US wataka kashfa za ngono za Trump zichunguzwe
Dec 12, 2017 04:48Makumi ya wabunge wanawake wa chama cha Democratic nchini Marekani wameitaka Kamati ya Usimamizi ya Bunge la nchi hiyo ianzishe uchunguzi mara moja kuhusu tuhuma za unyanyasaji wa kingono zinazomuandama Rais Donald Trump wa nchi hiyo.
-
Trump, White House watengwa kutokana na uamuzi dhidi ya Quds
Dec 12, 2017 04:47Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon amesema kitendo cha Donald Trump cha kuitangaza Quds ambayo ina Kibla cha Kwanza cha Waislamu kuwa eti ni mji mkuu wa Israel imeifanya Ikulu ya White House na rais huyo wa Marekani watengwe kimataifa.
-
Rais wa Iran: Uamuzi usio sahihi wa Trump ni sawa na kumwagia petroli kwenye moto
Dec 10, 2017 13:05Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, uamuzi wa hivi karibuni wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kuitangaza Beitul-Muqaddas kuwa mji mkuu wa Israel na kutoa amri ya kuhamishiwa ubalozi wa Washington katika mji huo ulikuwa sawa na kumwagia mafuta ya petroli katika moto katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Silaha za Marekani na Israel zapatikana katika ngome za ISIS, Syria
Dec 10, 2017 03:48Siku chache baada ya Mkuu wa Jeshi la Russia kutangaza kuwa genge la kigaidi la Daesh (ISIS) limeangamizwa kikamilifu nchini Syria, shehena ya silaha zilizotengenezewa Marekani na Israel imepatikana na wanajeshi wa Syria katika mji wa Dayr al-Zawr, iliyokuwa ngome ya mwisho ya magaidi hao.