-
Mkutano wa Miujiza ya Kisayansi wa Qur'ani waanza Misri
Mar 13, 2018 12:11Mkutano wa Kumi wa Muujiza wa Kisayansi katika Qur'ani na Suna umeanza katika Chuo Kikuu cha Mansoura kilichoko umbali wa kilomita 120 kaskazini mashariki mwa mji wa Cairo nchini Misri.
-
Rais wa Sudan aonana na Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Misri
Mar 11, 2018 22:59Rais Omar al Bashir wa Sudan ameonana na Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Misri mjini Khartoum na kujadiliana naye masuala mbalimbali yanayozihusu nchi hizo mbili.
-
Mashambulizi mapya yasababisha kuuawa askari 2 na magaidi 16 Sinai, Misri
Mar 11, 2018 12:47Wimbi jipya la mapigano katika Rasi ya Sinai nchini Misri limepelekea kuuawa wapiganaji 16 wa kundi la kigaidi na wanajeshi wawili wa serikali.
-
Zaidi ya magaidi 100 wauawa katika Rasi ya Sinai nchini Misri
Mar 09, 2018 00:26Msemaji wa jeshi la Misri ametangaza habari ya kuangamizwa zaidi ya magaidi mia moja katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita kwenye jimbo la Sinai, kaskazini mwa nchi hiyo.
-
UN yakosoa ukandamizaji Misri kuelekea uchaguzi wa rais
Mar 07, 2018 22:10Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amekosoa mazingira ya vitisho, ukandamizaji na kuwekewa mbinyo wanasiasa wa upinzani nchini Misri kuelekea uchaguzi wa rais unaotazamiwa kufanyika baadaye mwezi huu.
-
Bahram Qassemi ajibu tuhuma za Saudia na Misri dhidi ya Iran
Mar 07, 2018 11:47Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Bahram Qassemi sambamba na kutupilia mbali tuhuma za kujikariri dhidi ya taifa hili zilizotolewa katika ripoti ya pamoja ya Saudia na Misri, amesema kuwa tuhuma hizo hazina msingi, ni za kubuni na ni makosa haribifu ya kukaririwa.
-
Kundi moja la kigaidi lasambaratishwa nchini Misri
Mar 04, 2018 13:36Duru za usalama za nchini Misri zimetangaza habari ya kusambaratishwa kundi moja la kigaidi lenye mfungamano na Daesh (ISIS) katika mkoa wa Minya, kusini mwa mji mkuu Cairo.
-
Mahakama Misri yaidhinisha Saudia kupewa visiwa vya nchi hiyo
Mar 04, 2018 04:25Mahakama ya Juu nchini Misri imefutilia mbali maamuzi yaliyotolewa na mahakama za chini za nchi hiyo kuhusu mpango wa kukabidhi visiwa viwili vya kistratajia vya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kwa Saudi Arabia.
-
Magaidi 13 wengine waangamizwa Sinai Misri
Mar 01, 2018 12:01Jeshi la Misri limetangaza habari ya kuangamizwa magaidi 13 katika muendelezo wa operesheni za wanajeshi wa nchi hiyo katika Rasi ya Sinai.
-
Mwendesha mashtaka wa Misri ataka kufuatiliwa vyombo vya habari nchini humo
Feb 28, 2018 13:01Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Misri ametaka kufuatiliwa kwa kina na kwa karibu shughuli za vyombo vya habari na kuchukuliwa hatua za kisheria dhidi ya chombo chochote cha habari ambacho kinavuruga usalama na kuhatarisha maslahi ya taifa.