-
Misri yakosoa hatua ya baadhi ya nchi katika kuunga mkono ugaidi
Apr 12, 2017 09:41Waziri Mkuu wa Misri amezituhumu baadhi ya nchi waungaji mkono wakubwa wa makundi ya kigaidi.
-
Larijani: Lengo la makundi ya kigaidi ni kuzusha udini duniani
Apr 11, 2017 10:52Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amelaani vikali mashambulizi ya kigaidi dhidi ya makanisa mawili nchini Misri siku ya Jumapili iliyopita ambapo makumi ya watu waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa huku akisisitiza kuwa, lengo la magaidi ni kuzusha mifarakano ya kidini duniani.
-
Siku ya Umwagaji Damu nchini Misri
Apr 10, 2017 08:33Jumapili ya jana Misri ilikumbwa na hujuma za kigaidi zilizojumuisha milipuko minne ambapo watu karibu 47waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
-
Iran yalaani mashambulizi ya kigaidi dhidi ya Makanisa Misri
Apr 10, 2017 03:06Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali mashambulizi ya kigaidi dhidi ya makanisa mawili nchini Misri hapo jana, ambapo makumi ya watu waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
-
Rais wa Misri alitaka jeshi kulinda usalama wa maeneo muhimu
Apr 10, 2017 02:38Rais Abdel Fattah el-Sisi wa Misri ametaka kuwekwa haraka vikosi vya ulinzi katika maeneo muhimu kwa ajili ya kulisaidia jeshi la polisi katika kulinda usalama wa miundombinu muhimu kwenye mikoa yote ya nchi hiyo.
-
Hizbullah na Hamas zalaani hujuma za kigaidi dhidi ya makanisa huko Misri
Apr 09, 2017 23:48Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya nchini Lebanon imelaani vikali miripuko ya kigaidi katika makanisa mawili nchini Misri iliyosababisha mauaji, na kwamba hujuma hizo dhidi ya Wakristo ni za kishenzi.
-
Wimbi la mlipuko wa mabomu dhidi ya makanisa laua makumi nchini Misri
Apr 09, 2017 09:27Watu wasiopungua 140 wameuawa na kujeruhiwa katika wimbi la mashambulizi ya mabomu yaliyolenga makanisa nchini Misri hii leo.
-
Mahakama ya Misri yatengua uamuzi uliozuia kutolewa visiwa vya nchi hiyo kwa Saudia
Apr 03, 2017 00:08Mahakama moja ya Misri imetengua uamuzi uliotolewa miezi kadhaa iliyopita na mahakama nyingine ya nchi hiyo ikipinga kutolewa visiwa viwili vya nchi hiyo kwa utawala wa Saudi Arabia
-
Mufti wa Misri: Fatwa 3000 zimetolewa kupinga kuishi pamoja Waislamu na Wakristo
Apr 01, 2017 11:55Mufti wa Misri amesema kuwa asilimia 90 ya hukumu na fatwa za watu wanaofurutu ada zinawachochea watu kwenda kinyume na maamrisho ya Mwenyezi Mungu na kuzusha mifarakano baina ya Waislamu na Wakristo.
-
Magaidi watano wauawa, 16 watiwa mbaroni kaskazini mwa Misri
Mar 26, 2017 09:11Jeshi la Misri leo limetoa taarifa na kusema kuwa, limefanikiwa kuua magaidi watano na kuwatia mbaroni wengine 16 katika operesheni maalumu iliyofanywa na jeshi hilo kaskazini mwa Misri.