-
Waislamu Nigeria waendelea kuandamana kutaka Sheikh Zakzaky aachiliwe huru
Nov 28, 2018 23:40Wananchi Waislamu wa Nigeria wamefanya maandamano ya kutaka kiongozi wa harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo Sheikh Ibrahim Zakzaky aachiliwe huru.
-
Boko Haram yawateka nyara watema kuni 50 Nigeria
Nov 23, 2018 04:26Kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram limeripotiwa kuwateka nyara makumi ya watu waliokuwa wanatema kuni kaskazini mashariki mwa Nigeria, karibu na mpaka wa nchi hiyo na Cameroon.
-
Jeshi la Nigeria lakosolewa kwa 'kumuua mara mbili' kamanda wa Boko Haram
Nov 20, 2018 04:34Waandishi wa habari, wakosoaji wa serikali na watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini Nigeria wamelijia juu jeshi la nchi hiyo kwa kutangaza kuwa limemuua kamanda mwandamizi wa kundi la kigaidi la Boko Haram, licha ya kutoa taarifa kama hiyo mwaka jana.
-
Waislamu Nigeria waendeleza maandamano kutaka Sheikh Zakzaky aachiliwe
Nov 17, 2018 23:15Waislamu nchini Nigeria wameendeleza maandamano katika mji mkuu, Abuja, kulalamikia kuendelea kushikiliwa kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini humo Sheikh Ibrahim Zakzaky.
-
Wanafunzi Waislamu Nigeria waruhusiwa kuvaa Hijabu shuleni Lagos
Nov 15, 2018 11:56Baraza Kuu la Masuala ya Kiislamu Nigeria NSCIA limepongeza agizo la Mahakama ya Juu nchini humo la kuitaka serikali ya jimbo la Lagos kuwaruhusu wanafunzi Waislamu kuvaa Hijabu katika shule za umma katika mji mkuu huo wa kibiashara.
-
Boko Haram yaua wakulima 16 Borno, kaskazini mwa Nigeria
Nov 14, 2018 11:00Kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram limeshambulia vijiji kadhaa katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria na kuua wakulima wasiopungua 16.
-
Waislamu Nigeria waandamana kulaani mauaji yaliyofanywa na jeshi
Nov 14, 2018 04:50Waislamu Nigeria wameandamana nje ya ofisi za Tume ya Haki za Binaadamu katika mji mkuu Abuja, kulaani mauaji yaliyofanyika kati ya 27 hadi 30 Oktoba mwaka huu.
-
Makumi ya watu waripotiwa kuaga dunia Nigeria kwa kipindupindu
Nov 12, 2018 23:22Kamisheni ya Wakimbizi ya Norway imetangaza kuwa idadi ya maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu yameshika kasi zaidi huko kaskazini mwa Nigeria ambako makumi ya maelfu ya raia wamelazimika kukimbia makazi yao kutokana na mashambulizi yanayofanywa na kundi la kigaidi la Boko Haram.
-
Mamia ya raia wakimbia baada ya shambulio la Boko Haram Nigeria
Nov 12, 2018 04:16Mamia ya wanavijiji juzi jioni walizikimbia nyumba zao huko kaskazini mashariki mwa Nigeria baada ya wanamgambo wa kundi la Boko Haram kuwashambulia.
-
UNHCR: Zaidi ya Wacameroon 30,000 wamekimbilia nchini Nigeria
Nov 10, 2018 10:43Msemaji wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) amesema kuwa, idadi ya raia wa Cameroon waliokimbilia nchini Nigeria kukwepa machafuko katika nchi yao imeongezeka na kupindukia 30,000.