-
Mahakama Nigeria yakataa kumuachia huru kwa dhamana Sheikh Zakzaky
Nov 08, 2018 01:18Mahakama nchini Nigeria imekataa kumwachia huru kwa dhamana kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya nchini humo Sheikh Ibrahim Zakzaky siku kadhaa baada ya wafuasi wake zaidi ya 40 kuuawa katika maandamano waliyofanya kutaka kuachiwa huru kiongozi huyo wa kidini.
-
Amnesty International yakiri kuuawa kinyama Mashia wa Nigeria
Nov 01, 2018 01:09Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch limevinyooshea kidole cha lawama vikosi vya usalama vya Nigeria likivituhumu kwamba, vimehusika na mauaji ya kinyama ya makumi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini humo.
-
Jeshi la Nigeria laendeleza jinai dhidi ya Mashia, lawafyatulia risasi na kuwaua waandamanaji kadhaa
Oct 30, 2018 03:57Jeshi la Nigeria, kwa mara nyengine tena limewashambulia kwa kuwafyatulia risasi Waislamu wa madhehebu ya Shia waliokuwa wakiandamana katika mji mkuu wa nchi hiyo Abuja na kuwaua shahidi waandamanaji kadhaa.
-
Jeshi la Nigeria laua Waislamu 10 wakishiriki Arubaini ya Imam Hussein AS
Oct 27, 2018 23:32Wanajeshi wa Nigeria wameushambulia msafara wa Waislamu wa madhehebu ya Shia waliokuwa wakishiriki katika maombolezo ya Arubaini ya Imam Hussein AS, viungani mwa mji mkuu wa nchi Abuja, na kuua shahidi kumi miongoni mwa waumini hao.
-
Nigeria yaweka amri ya kutotoka nje mjini Kaduna baada ya mapigano ya kikabila kuua watu 55
Oct 23, 2018 03:25Maafisa wa serikali ya Nigeria wametuma kikosi maalumu cha polisi katika jimbo la Kaduna la kaskazini mwa nchi hiyo na kutangaza amri ya masaa 24 ya kutotoka nje baada ya kutokea mapigano ya kikabila yaliyoua makumi ya watu.
-
Watu 55 wauawa katika mapigano ya kidini nchini Nigeria
Oct 21, 2018 10:18Watu wasiopungua 55 wameuawa katika mapigano ya kidini jimboni Kaduna, kaskazini magharibi mwa Nigeria.
-
Wakulima 12 wauawa na magaidi wa Boko Haram katika jimbo la Borno
Oct 21, 2018 04:14Kundi la kigaidi la Boko Haram limewaua wakulima wasiopungua 12 na kujeuhi makumi ya wengine, baada ya kufanya shambulio katika kitongoji kimoja katika mji wa Maiduguri ulioko katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
UN: Kundi la wanamgambo la Nigeria lamewaachia watoto 833
Oct 12, 2018 13:31Kundi moja la wanamgambo ambalo linaendesha mapambano dhidi ya kundi la kigaidi la Boko Haram kaskazini mwa Nigeria limewaachia huru watoto 833 miongoni mwa ngazi zake.
-
Waziri wa zamani wa Nigeria na mfuatiliaji wa hatima ya mabinti wa Chibok kugombea urais
Oct 07, 2018 11:45Bi Obiageli Ezekwesili Waziri wa zamani wa Nigeria na mwasisi mwenza wa kundi linalofuatilia mahali walipo mabinti zaidi ya 200 waliotekwa nyara mwaka 2014 na kundi la kigaidi la Boko Haram leo ametangaza nia yake ya kuwania kiti cha urais mwakani.
-
Mamia ya Wanigeria wafanya tena maandamano mjini Abuja kutaka kuachiliwa huru Sheikh Zakzaky
Oct 06, 2018 11:36Waislamu nchini Nigeria wamefanya tena maandamano kulalamikia kuendelea kushikiliwa kiongozi wao Sheikh Ibrahim Zakzaky ambaye bado yuko jela licha ya Mahakama Kuu ya Nigeria kutoa amri ya kuchiliwa huru mwaka 2016.