-
Israel yatenga $18M za ujenzi wa vitongoji vipya Palestina
Jun 20, 2016 02:38Utawala haramu wa Israel umeidhinisha dola milioni 18 za Marekani zitakazotumiwa katika ujenzi wa vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Wapalestina unazozikalia kwa mabavu.
-
HAMAS: Tuna matumaini ya kivuko cha Rafah kufunguliwa moja kwa moja
Jun 17, 2016 00:12Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema wana matumaini ya kufunguliwa moja kwa moja kivuko cha Rafah ambacho ni kivuko muhimu zaidi kinachounganisha eneo la Ukanda wa Gaza, Palestina na ulimwengu wa nje.
-
Israel yawakatia maji Wapalestina Ukingo wa Magharibi
Jun 15, 2016 02:48Utawala wa Kizayuni wa Israel umewakatia huduma za maji Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan licha ya joto kali na hitajio kubwa la bidhaa hiyo muhimu katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
-
HAMAS: Kuwatia mbaroni Wapalestina kutashamirisha Intifadha
Jun 11, 2016 11:00Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imesistiza kuwa kitendo cha askari wa utawala wa Kizayuni cha kuwatia nguvuni Wapalestina kitashamirisha na kupanua zaidi Intifadha ya Quds.
-
UN yaikosoa Israel kuwakataza Wapalestina kuingia katika ardhi zao
Jun 10, 2016 23:19Umoja wa Mataifa umeukosoa utawala haramu wa Israel kwa kuwazuia Wapalestina kuingia na kutembea katika ardhi zao unazozikalia kwa mabavu.
-
Israel yawakataza Wapalestina kutembeleana mwezi wa Ramadhan
Jun 09, 2016 09:25Utawala wa Kizayuni wa Israel umewapiga marufuku Wapalestina kutembeleana na kufanya ziara katika maeneo matakatifu ya ardhi zao zinazokaliwa kwa mabavu, katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan, kufuatia shambulizi dhidi ya Tel Aviv.
-
Palestina: Ni kinaya kuteuliwa Israel kuongoza kamati ya UN
Jun 08, 2016 23:12Afisa wa ngazi za juu wa Palestina ameitaja kama kichekesho na kinaya, hatua ya kuteuliwa utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Mataifa.
-
Radiamali mbalimbali kuhusu kimya cha nchi za Kiarabu mbele ya jinai za Israel
Jun 08, 2016 01:40Harakati ya Hizbullahi ya Lebanon imelaani kimya cha nchi za Kiarabu mbele ya jinai za Wazayuni na kusema kukwa, kimya hicho ni mkamilishaji wa siasa za kuwa na uhusiano wa kawaida kati ya nchi hizo na Israel.
-
Walowezi wa Kizayuni wafanya maandamano Quds, wavamia al-Aqsa
Jun 06, 2016 02:59Maelfu ya walowezi wa Kizayuni wamefanya maandamano ya kutiliwa shaka mashariki mwa Quds inayokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel na kuzusha hali ya taharuki katika eneo hilo.
-
Jeshi la Israel lamuua shahidi mwanamke wa Palestina
Jun 02, 2016 10:21Askari wa jeshi katili la utawala haramu wa Israel wamemuua shahidi mwanamke wa Kipalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan hii leo.