-
UN: Myanmar haipo tayari kuwapokea wakimbizi Warohingya
Apr 08, 2018 07:27Umoja wa Mataifa umesema Myanmar haipo tayari kuwapokea malaki ya wakimbizi Waislamu wa Rohingya wanaoishi kambini katika nchi jirani ya Bangladesh.
-
Nchi za Asia zambana kiongozi wa Mynamar kuhusu mauaji ya Warohingya
Mar 18, 2018 16:25Viongozi wa nchi za Asia na Australia wamemjia juu kiongozi wa Myanmar kutokana na kutochukua hatua za maana serikali yake kukomesha wimbi la mauaji ya Waislamu wa jamii ya Rohingya mkoani Rakhine.
-
Umoja wa Mataifa watoa wito wa kusaidiwa wakimbizi Waislamu Warohingya
Mar 17, 2018 07:59Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kukusanywa misaada kwa ajili ya kuwasaidia wakimbizi takribani milioni moja wa jamii ya Rohingya wa Myanmar ambao wako katika kambi za wakimbizi nchini Bangladesh sambamba na kuandaliwa mazingira ya Waislamu hao kurejea nchini kwao.
-
Wataalamu wa UN: Facebook imechangia mauaji ya Waislamu wa Rohingya
Mar 13, 2018 17:21Wataalamu wa masuala ya haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wameulaumu mtandao wa kijamii wa Facebook kwa kuruhusu uchochezi wa machafuko na ukatili dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar.
-
Amnesty International : Jeshi la Myanmar linatwaa maeneo ya Waislamu Warohingya
Mar 12, 2018 07:24Utafiti mpya uliofanywa na Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International unaonyesha kuwa, jeshi la Myanmar limejenga kituo katika vijiji ambavyo Waislamu wa jamii ya Rohingya wamelazimishwa kuyakimbia makaazi yao.
-
UN: Tuna wasi wasi mauaji ya kimbari yamefanyika Myanmar
Mar 08, 2018 01:41Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ameeleza juu ya wasi wasi mkubwa alionao kwamba yumkini mauaji ya kimbari yamefanywa dhidi ya Waislamu wa Rohingya nchini Myanmar tangu Agosti mwaka jana 2017.
-
UN yasema mauaji dhidi ya Waislamu wa Rohingya yanaendelea Myanmar
Mar 06, 2018 07:58Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imetahadharisha kuhusiana na kuendelea mauaji ya kizazi yanayofanywa na serikali ya Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya magharibi mwa nchi hiyo.
-
MSF: Waislamu wa Rohingya wangali wanamiminika Bangladesh
Feb 21, 2018 03:12Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) imetangaza kuwa, mamia ya wakimbizi wa jamii ya Waislamu wa Rohingya wanaokimbia ukatili na mauaji nchini Myanmar wangali wanamiminika katika nchi jirani ya Bangladesh na kwamba mgogoro wa Rohingya bado unaendelea.
-
Kuwasilishwa kwa Myanmar orodha ya kwanza ya Waislamu wa Rohingya watakaorejeshwa nchini humo
Feb 18, 2018 08:13Waziri wa Mambo ya Ndani wa Bangladesh ameikabidhi Myanmar orodha ya kwanza ya wakimbizi wa Waislamu wa kabila la Rohingya ambao wanatazamiwa kurejeshwa katika makazi yao.
-
UN: Myanmar haijaandaa mazingira salama ya kurejea nchini Warohingya
Feb 14, 2018 07:25Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) amesema Myanmar imeshindwa kuandaa mazingira salama ya kuruhusu kurejea kwa khiari nchini humo Waislamu wakimbizi 688,000 Warohingya waliokimbilia nchi jirani ya Bangladesh.