-
Katibu Mkuu wa CUF avunja ukimya kuhusu upekuzi wa polisi Makao Makuu Mtendeni Zanzibar + Sauti
Mar 01, 2018 13:26Katibu Mkuu Taifa wa chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema kuwa matukio ya hivi karibuni ya jeshi la polisi ya kupekua makao makuu ya chama hicho huko Mtendeni mjini Unguja na ziara ya kisiwani Pemba ya yule anayejiita Mwenyekiti wa chama hicho, yalikuwa na lengo la kusababisha vurugu. Taarifa kamili anatuletea mwandishi wetu wa visiwani Zanzibar, Harith Subeit.
-
Jaji Mkuu wa Kenya awaomba radhi wananchi + Sauti
Mar 01, 2018 13:13Jaji wa Mahakama Kuu ya Kenya David Kenani Maraga, amewaomba radhi Wakenya kwa niaba ya idara hiyo kufuatia kuendelea kuzuiliwa baadhi ya washukiwa wa uhalifu walio na akili punguani katika magereza ya nchi hiyo.
-
Utitiri wa makanisa nchini Rwanda wawachosha wananchi
Feb 21, 2018 02:15Wananchi wa matabaka mbalimbali na wa dini tofauti nchini Rwanda wamelalamikia ujenzi mkubwa wa kiholela wa makanisa nchini humo ambao wanasema umewachosha hususan kutokana na vipaza sauti vinavyotumiwa na makanisha hayo katika makazi ya raia. Mwandishi wa Radio Tehran, Sylvanus Karemera, ametuandalia ripoti maalumu kuhusu suala hilo...
-
Upekuzi wa polisi katika Ofisi Kuu ya CUF Zanzibar wamalizika salama + Sauti
Feb 19, 2018 14:56Upekuzi uliofanywa na Jeshi la Polisi Zanzibar katika Makao Makuu ya chama cha CUF, Mtendeni Kisiwani Unguja umemalizika kwa jeshi hilo kutangaza kuwa halikupata silaha wala miripuko iliyodaiwa kufichwa katika ofisi hiyo. Harith Subeit ametuandalia ripoti kuhusu tukio hilo
-
Madaktari wanajeshi wa EAC wakutana Kigali + Sauti
Feb 19, 2018 14:48Wanajeshi madaktari kutoka wizara za ulinzi kwenye mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wamekutana mjini Kigali kujadili changamoto za afya na huduma ya matibabu kwenye majeshi ya nchi zote za jumuiya ya Afrika mashariki Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylivaus Karemera anaripoti zaidi
-
Ziara ya wabunge wa Afrika Mashariki nchini Burundi + Sauti
Feb 19, 2018 14:43Wabunge kadhaa wa Jumui ya Afrika Mashariki wamefanya ziara ya kutembelea maeneo tofauti ya Burundi kama sehemu ya juhudi za kuimarisha uchumi wa nchi za ukanda huo. Mwandishi wa Radio Tehran jijini Bujumbura, Hamida Issa na maelezo zaidi...
-
Mahakama Uganda yamnusuru mwandishi aliyetekwa nyara + Sauti
Feb 19, 2018 14:31Mahakama moja nchini Uganda imemnusuru mwandishi mwandamizi wa gazeti la serikali la New Vision aliyetekwa nyara hivi karibuni.
-
Wadadisi wa mambo wakosoa uchaguzi mdogo wa Tanzania + Sauti
Feb 18, 2018 13:19Wachambuzi wa kisiasa wamekosoa mienendo ya dola katika uchaguzi huo wa Kinondoni na Siha
-
Kongamano la Kiislamu Kampala lawahimiza Waislamu kupendana + Sauti
Feb 11, 2018 03:23Walimwengu wa leo wanajijazia ugumu wenyewe kwa kuacha kufuata mafundisho matukufu ya Mwenyezi Mungu ikiwa ni pamoja na kuacha kupenda, kinyume kabisa na mafundisho ya Uislamu. Hayo yamesemwa katika kongamano maalumu la Waislamu lililofanyika mjini Kampala Uganda. Mwandishi wetu Kigozi Ismail ametuandalia ripoti ifuatayo:
-
Chadema yalalamikia "udanganyifu" uchaguzi mdogo wa Kinondoni, Siha + Sauti
Feb 08, 2018 04:12Chama cha upinzani nchini TanzaniaCHADEMA kimesema hakiridhishwi na mwenendo wa haki katika nyanja ya demokrasia kutokana na mlimbikizo wa matukio yanayoonesha ukandamizwaji wa vyama vya upinzani nchini humo.